• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

Dkt. Mahenge awataka wakandarasi kumaliza miradi ya madaraja kabla msimu wa mvua haujafika.

Posted on: August 10th, 2021

Mkuu wa Mkoa Singida Mhe. Dkt. Binilith Mahenge amewataka TANROAD kumaliza haraka ujenzi wa daraja unaoendelea katika Kata ya Msingi Wilayani Mkalama mkoani hapa ili kurahisisha mawasiliano  katika maeneo mbalimbali  kabla msimu wa mvua haujaanza.

Dkt. Binilith Mahenge ametoa maelekezo hayo leo tarehe 10.08.2021 alipotembelea mradi wa ujenzi wa daraja lililopo   Kata ya Msingi wilaya ya Mkalama ambapo amesema daraja hilo likikamilika litaweza kuhudumia mikoa ya Mwanza, Simiyu na Manyara.

Aidha amewapongeza viongozi wa TANROAD mkoani hapo kwa usimamizi mzuri wa ujenzi huo na kuwataka kuhakikisha kwamba daraja linakamilika kwa ubora na muda uliopangwa.

Hata hivyo RC amebainisha kwamba kumalizika kwa ujenzi wa daraja hilo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 10.9 na linatakiwa kukamilika ifikapo tarehe 30.10.2021.

Aidha Mhe. Dkt. Mahenge amewapongeza Viongozi wa TANROAD  kwa usimamizi mzuri pamoja na changamoto za mvua kwa msimu uliopita lakini kazi imeendelea kuwa nzuri.

Amesema kukamilika kwa daraja hilo kutahamasisha  kwa kiasi kikukbwa ukuaji wa uchumi wa mtu mmoja mmoja na  taifa kwa ujumla.

“Nimefahamishwa kwamba daraja hili linaunganisha mikoa ya Simyu, Mwanza, Manyara na kwa mkoa wa Singida linaunganisha Wilaya ya Mkalama na Iramba, ni matumaini yangu kwamba shughuli za uchumi zitaimarika sana kwa mtu mmoja na Taifa kwa ujumla wake” Alisema Dkt. Mahenge.

Awali akimkaribisha RC, Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe.  Sophia Mfaume Kizigo amesema daraja hilo ambalo ni kiungo muhimu cha wilaya ya Mkalama na Iramba litawasidia wananchi wa maeneo hayo kuendesha shughuli za kila siku kwa ufasaha kutoka eneo moja kwenda jingine.

Aidha ufanikishwaji wa daraja hilo utasababisha barabara nyingine zinazounga wilaya na mikoa mbalimbali kujengwa kwa kiwango cha lami alisistiza Mhe.  Sophia

Naye Diwani wa Kata ya Msingi wilayani hapo Mhe. Amri Juma  ameishukuru Serikali kwa jitihada za kufanikisha ujenzi wa daraja hilo na mengine madogo yanayojengwa na TARURA katika Kata hiyo kwamba ni ishara ya mabadiliko makubwa ya kiutendaji unaofanywa na Serikali ya awamu ya sita.

Naye Mhandisi Deus Masige Meneja wa TANROAD mkoani Singida amesema daraja linaurefu wa mita 100 na midomo ya kupitisha maji  mnne (4)  ambapo limefikia asilimia 67 na linatumia fedha za ndani.

Ujenzi wa daraja hilo ulitegemewa kumalizika   tarehe 11/12/2020 lakini kutokana na changamoto za mvua kwa msimu uliopita halikuweza kumalizika kwa wakati.

Mwisho Mhandisi Masige amemhakikishia Mkuu wa mkoa kwamba pamoja na changamoto zilizojitokeza lakini ujenzi wa daraja hilo utakamilika ifikapo 30/10/2021.

Mkuu wa Mkoa Singida Mhe. Dkt. Binilith Mahenge akitoa maelekezo kwa meneja wa TANROAD Mhandisi Deus Masige mkoa wa Singida baada ya kutembelea ujenzi wa daraja, pembeni ni Mkuu wa wilaya ya Mkalama Mhe. Sophia Mfaume Kizigo

Katika hatua nyingine Mhe. Dkt. Binilith Mahenge amewataka wananchi wa Mkalama na maeneo mengine kujikinga na ungojwa wa Covid 19 na kuendelea kupata chanjo ambazo Serikali imeshazisambaza maeneo mbalimbali mkoani hapo.

Amesema Mkoa umepokea chacho Zaidi ya 30,000 ili wananchi waweze kupata  chanjo hizo ambazo Serikali imejiridhisha kwamba ni salama kwa afya ya watu wake.

Aidha Mhe. Dkt. Mahenge amewaagiza wakuu wa wilaya zote mkoani hapo kuendelea kuhamasisha wananchi kupata chanjo ya korona kama sehemu ya mapambano dhidi ya ugonjwa huo.

Amewataka madiwani kusaidia kutoa elimu kwa wananchi kuhusu misongamono ambayo sio ya lazima ili kuepuka usambazaji wa ugonjwa huo endapo mtu mmoja atakuwa ameathirika.

Naye Mzee Aroni Msindye Mwenyekiti wa Baraza la wazee wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani hapo ameiomba Serikali kusogeza karibu vituo vya kupatia chanjo ili wazee waweze kufika kwa urahisi.

Mzee Aroni amebainisha kwamba wazee kwa sasa wanapata changamoto ya umbali hivyo wengi kushindwa kupata chanjo hiyo.

Imeandaliwa na 

Afisa Habari

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida

http://singidars.blogspot.com/

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.