• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

"Endeleeni kuandaa mashamba mbolea inakuja"- Serukamba.

Posted on: November 28th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amewataka Wakulima Mkoani Singida kuendelee kuandaa mashamba kwa ajili ya kilimo wakati Serikali ikiendelea na mchakato wa kuleta mbolea ya kutosha katika Wilaya mbalimbali.

Kauli hiyo ameitoa leo katika Kikao kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi hiyo ambacho  kiliwakutanisha Wakuu wa Wilaya, Wakurungenzi na Maafisa kilimo wa Halmashauri zote Mkoani lengo likiwa ni kujadili changamoto mbalimbali ikiwemo upatikanaji wa mbolea, Maandalizi ya mashamba darasa na mashamba darasa pamoja na changamoto za wadaiwa.  

RC Serukamba amewataka wakulima kuendelea na maandalizi ya msimu wa kilimo kwa kuwa swala la upatikanaji wa mbolea linashughulikiwa na viongozi wa Serikali kuhakikisha mbolea inamfikia kila mkulima huku akiwataka Wakuu wa Wilaya kuendelea kuwakumbusha wahusika mara kwa mara.

Awali akichangia mada juu ya hali ya upatikanaji wa mbolea Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskasi Muragili amesema Wakulima wa Wilaya yake wana uhitaji mkubwa wa mbolea kwa ajili ya Kilimo hivyo zifanyike juhudi mbalimbali kuhakikisha Mawakala wanaleta mbolea ya kutosha kwa wakati.

Aidha Muragili ameeleza kwamba uwezo wa Mawakala kununua kiasi kikubwa cha mbolea ni mdogo jambo ambalo limesababisha hofu kwa Wakulima kukosa mbolea wakati msimu ukiwa umekaribia.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Jerry Muro, ameeleza kwamba Wilaya hiyo mpaka sasa hakuna mbolea iliyoingia jambo ambalo limekuwa likilalamikiwa na Wakulima.

Jerry ameeleza kwamba Wakulima Wilayani hapo walishakamilisha maandalizi ya msimu wa kilimo kwa kupata mbegu na kusafisha mashamba jambo lililobaki ni kuwa na uhakika wa mbolea tu alieleza.

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Suleimani Mwenda, akizungumza wakati wa kikao hicho.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Iramba Suleimani Mwenda, amesema wao wameweza kupata mbolea kwa kiasi kikubwa kwa sababu wakulima walikuwa tayari wameshachanga fedha hivyo kuwafanya wa mawakala wa mbolea kupata kushawishika zaidi.

Amesema kununua Mawakala wengi hawana mtaji mkubwa hivyo wakihakikishiwa fedha wanaweza kuleta eneo lolote ili waweze kupata fedha na kuagiza mzigo mwingine.

Akihitimisha mjadala huo Mkuu wa Mkoa amesema Serikali ipo makini katika zoezi la usambazaji wa mbolea ili kuepusha uvushaji wa mbolea hiyo kwenda nje ya nchi kwa kuwa imeweka fedha nyingi za ruzuku.

Mwisho

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.