• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

"FIKIRIENI KUJIAJIRI BAADA YA KUHITIMU"- DENDEGO

Posted on: November 22nd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Singida Halima Dendego amewashauri wahitimu wa taasisi ya Uhasibu Tanzania kufikiri zaidi kujiajiri badala ya kutegemea ajira za serikali na  sekta binafsi.

Mhe.Dendego amesema hayo katika mahafali ya 22 ya chuo cha Uhasibu Tanzania tawi la Singida. , na mahafali ya 13 ya Tawi la Singida, yaliyofanyika chuoni hapo kuanzia ngazi ya cheti hadi uzamili.

“ Nawaomba mfikirie zaid kujiajiri kuliko kuajiriwa vipaji mnavyo kama nilivyoona wanafunzi wakibuni mbinu mbalimbali za biashara kwani licha ya ajira kutoa fursa nzuri lakini kujiajiri kunatoa nafasi ya kuwa mbunifu na uhuru wa kufikia malengo yaliyokusudiwa"alisema Mhe.Dendego.

Akiongelea kuhusu wahitimu 1477 waliohitimu katika fani mbalimbali amesema idadi hiyo ni kubwa na faraja kubwa kwa Mkoa wa Singida hivyo wakiitumia katika kutengeneza ajira kutaleta mabadiliko

Kuhusu baadhi ya wanachuo wanao onyesha ubunifu, Mkuu  wa Mkoa amesema serikali ya mkoa itashirikiana nao kwa karibu ili kuhakikisha wanafikia malengo yao huku akiwataka kutumia mitandao ya kijamii kama jukwaa la kutangaza ubunifu, kukutana na wateja, na kueneza mawazo mapya Badala ya kupoteza muda mitandaoni kwa mambo yasiyokuwa na manufaa kwani mitandao hiyo inatoa fursa kubwa ya kujitangaza, kukuza biashara, na kufikia mafanikio makubwa.

Awali,Mhe. Dendego alianza kwa kuzindua program ya  ‘Masters’ ambayo itapatikana katika kampasi ya Singida huku akipongeza juhudi zinazofanywa na Taasisi ya Uhasibu Nchini (TIA), katika kuboresha miundombinu na kusimamia maendeleo ya Tawi lake la Singida, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa jengo jipya la utawala litakalokuwa na ghorofa tano na kugharimu zaidi ya Shilingi bilioni 13.5.

Ameeleza kuwa maboresho hayo yanaashiria ukuaji wa chuo hicho na yanaongeza fursa kwa vijana kujifunza maarifa na ujuzi zaidi unaoendana na mahitaji ya soko la ajira.

“Serikali itaendelea kushirikiana na wanafunzi na uongozi wa chuo hiki. Nawaomba sana mkitumie chuo hiki kujipatia maarifa zaidi kwa ajili ya kuitumikia jamii katika kila nyanja,” alisema Dendego.

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa TIA, Profesa William Palangyo, alisema kuwa kuanzishwa kwa shahada ya uzamili katika Tawi la Singida ni hatua muhimu itakayochochea ongezeko la wanafunzi wanaotamani kujiunga na chuo hicho.

“Hadi sasa, tayari tumewasajili wanafunzi 66 kwa shahada ya uzamili, ambao wanaendelea kupata maarifa na ujuzi zaidi kwa manufaa yao binafsi na ya taifa kwa ujumla,” alisema Profesa Palangyo.

Naye Mjumbe wa Bodi ya TIA, Renatus Msangira, aliyemwakilisha Mwenyekiti wa Bodi hiyo, aliwahimiza wananchi kutumia fursa ya uwepo wa chuo hicho kwa kuongeza maarifa ambayo yataboresha maisha yao.

Jumla ya wahitimu 1,477 walitunukiwa vyeti vyao katika ngazi mbalimbali za masomo, zikiwemo cheti na stashahada kwenye fani za mahusiano ya umma, uhasibu, uongozi wa rasilimali watu, usimamizi wa biashara, pamoja na ununuzi na ugavi.



Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.