• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

Jiungeni katika vikundi ili mkopesheke - DC Muragili

Posted on: January 28th, 2022

Wafanyabiashara wadogo Manispaa ya Singida wameshauriwa kujiunga katika vikundi vya wajasiriamali na kuvisajili ili waweze kukopesheka katika taasisi mbalimbali za fedha.

Ushauri huo umetolewa leo Januari 28, 2022 na Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskasi Muragili wakati alipokutana na wafanyabiashara wadogo katika soko la wamachinga la Kata ya Majengo katika Manispaa hiyo alipokuwa akikabidhi fedha kiasi cha Tsh. 2,000,000 kwa niaba ya Mkuu wa mkoa huo .

Mhandisi Muragili amesema namna pekee ambayo vijana wataweza kupata mitaji kwa ajili ya kuendesha maisha yao ni kujiunga katika vikundi ili waweze kuaminiwa na kukopesheka.

Aidha DC Muragili amebainisha kwamba mabenki mbalimbali hapa Singida yakiwemo CRDB, NMB NBC na nyinginezo wameonesha utayari wa kuvikopesha vikundi ambavyo vimesajiliwa hivyo kuwataka vijana kujiunga ambapo Maafisa Maendeleo ya Jamii kusaidia utoaji wa miongozo mbalimbali kufanikisha zoezi hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskasi Muragili (mwenye suti) wakati alipokutana na wafanyabiashara wadogo katika soko la wamachinga la Kata ya Majengo katika Manispaa ya Singida. Wa kwanza kutoka kushoto ni Meya wa Manispaa ya Singida Yagi Maulid Kiaratu.

Amewakumbusha vijana wenye umri kati ya miaka 18 mpaka 35 kutumia fursa ya mikopo ya vijana asilimia nne(4%) inayotolewa na Halmashauri kwa kuwa ina mashart nafuu na haina riba.

Akitoa salamu za Mkuu wa Mkoa mbele ya wafanyabiashara hao (wamachinga) DC Paskasi amesema kiasi hicho cha fedha kimetolewa kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya usafi kama ambavyo alivyotoa ahadi hiyo alipokutana nao tarehe 06/11 mwaka jana.

Ununuzi wa vifaa hivyo ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo ya Mkuu wa Mkoa ya kufanya usafi kila jumamosi  katika maeneo yanayowazunguka ili kuepuka magonjwa ya milipuko alibainisha DC Muragili.

Katika hatua nyingine Mhandisi Paskasi  akawakabidhi fedha Tsh. 1,000,000 (Milioni moja ) kupitia kwa mwenyekiti wa Vijana Mtaa wa Majengo  Saidi Hassani kama sehemu ya ahadi ya mkuu wa Mkoa juu ya uboreshaji wa eneo lao la uoshaji wa magari.

DC akatumia muda huo kuwaasa vijana wote kutumia fedha hizo kwa malengo mahususi ili ziweze kuleta chachu katika biashara zao, na zisaidie kuibua miradi mipya ya maendeleo.

Sambamba na hilo DC Muragili akakabidhi shilingi milioni mbili(2,000,000) wa diwani wa Unyianga kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya Unyianga ikiwa ni muendelezo wa kukamilisha ahadi alizozitoa kwa wanachi.

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Singida Yagi Maulid Kiaratu amemshukuru Mkuu wa Mkoa huo kwa kutekeleza ahadi zake katika vikundi vilivyopo Kata ya Majengo na Kituo cha Afya Unyianga.

Meya huyo amewasihi Maafisa Maendeleo ya jamii ngazi ya wilaya kuendelea kufanya kazi kwa ukaribu na wafanyabiashara hao ili kusaidia kutambua fursa ambazo zinawazunguka .

Kwa pamoja viongozi hao wakatoa wito kwa wananchi kushiriki kikamilifu katika zoezi la upandaji miti litakalozindiuliwa ki mkoa jumamosi tarehe 29.01.2022 katika kingo za ziwa Kindai ili kurejesha mazingira ya ukijani mkoani Singida.

Baada ya uzinduzi huo kila mwananchi atatakiwa kupanda miti katika maeneo wanayoishi na maeneo ya mipaka ya mashamba yao kwa nyakati tofauti aliendelea kueleza Dc Muragili.

DC Muragili akikabidhi shilingi milioni mbili (2,000,000) kwa Diwani wa Unyianga kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya Unyianga ikiwa ni muendelezo wa kukamilisha ahadi alizozitoa Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge kwa wanachi.

Meya wa Manispaa ya Singida Yagi Maulid Kiaratu akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskasi Muragili  

Mtendaji wa Kata ya Majengo akisoma taarifa kwa Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Singida kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo wakati wa hafla ya utekelezaji wa ahadi ya Mkuu wa Mkoa kwa vijana 

Baadhi ya watendaji na vijana wa Kata ya Majengo wakati wa hafla ya utekelezaji wa ahadi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge kwa vijana hao.

Mwisho

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.