• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

Kamati ya Siasa Mkoani Singida Yafanya Ziara Manyoni, Itigi Watakaiwa Kukarabati Majengo Ya Zamani Ya Shule

Posted on: March 16th, 2022

Wananchi wa Mkoa wa Singida wametakiwa kuendelea kukarabati majengo ya zamani ya shule na vituo vya Afya vilivyopo mkoani hapo ili majengo hayo yaweze kuendelea kutumika kwa matumizi mbalimbali.

Wito huo umetolewa leo na Mwenyekiti  wa  Chama Cha Mapinduzi CCm Mkoa wa Singida Juma Kilimba wakati alipokuwa katika ziara ya kukagua na kupokea miradi ya maendeleo katika Wilaya ya Manyoni na Itigi.

Kilimba amesema kwamba Serikali imejenga Madarasa mapya 632 kupitia fedha za miradi ya maendeleo kwa Mkoa huo hivyo kuwataka Madiwani na viongozi wa vijiji na kata kusaidia usimamizi wa matumizi ya majengo hayo na kuwataka kuhakikisha ukarabati unafanyika katika madarasa ya zamani ili yaweze kuendelea na matumizi.

“Haina maana kwamba kwa kuwa tumepata madarasa mapya mengine ya zamani tuyaache bila kuyakarabati, viongozi wa vijiji na kata kwa kushirikiana na madiwani kuona namna ya kukarabati majengo ambayo yanaonekana kuwa yamechoka ili yaendelee kutumika”. Alisema Kilimba

Akitolea mfano wa mijadala iliyoibuliwa katika kikao cha ushauri wa mkoa (RCC) kilichofanyika hivi karibuni mkoani hapo Juma Kilimba amesema  mkoa umetafiti mbinu mbalimbali za kuimarisha viwango vya ufaulu, mbinu za kutumia TEHAMA  katika kuondoa changamoto ya uhaba wa walimu hivyo majengo hayo yatakuwa na kazi kubwa  endapo yatakarabatiwa.

Akiendelea na ukaguzi wa miradi mbalimbali Mwenyekiti huyo akaishukuru serikali ya awamu ya sita chini ya mama Samia Suluhu Hassani kwa kutoa kiasi kikubwa cha fedha ambapo katika kipindi cha mwaka 2022 wameweza kujenga miundombinu ya mabomba na kuchimba visima, ujenzi wa barabara za vijijini pamoja ujenzi wa vituo vya Afya.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa huo Dk. Binilith Mahenge akawataka ruwasa kuhakikisha wanajenga miundombinu ya maji iliyo imara ili kiuwasaidia wananchi kwa muda mrefu huku akiwakumbusha wataalamu hao kuhakikisha wanawasaidia wananchi waweze kuvuta maji majumbani mwao.

Aidha RC Mahenge akawataka wasimamizi wa miradi mbalimbali Mkoani hapo kuhakikisha kwamba fedha walizopewa zinatumika kama ilivyokubaliwa na kuleta tija kwa wananchi kwa kuwa lengo la serikali ni kuwanufaisha wananchi wake.

Wakiendelea na ukaguzi katika hospitali ya wilaya ya Manyoni Mwenyekiti wa halmashauri Jumanne Mlagaza pamoja na kuishukuru serikali kwa kuwapata fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya maendeleo, akamuomba mwenyekiti kusaidia wazo la kupata eneo la kujenga hospitali kubwa ya wilaya kwa kuwa eneo walilonalo kwa sasa ni dogo na halina miundombinu mizuri ya barabara na majengo ya kutosha.

Hata hivyo Jumanne akaendelea kusema kwamba  miradi yote inayotekelezwa katika Halmashauri ya Manyoni inategemewa kukamilika kwa wakati pamoja na uwepo wa changamoto za mvua na baadhi ya vitu kupanda bei.

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri wa Wilaya ya Manyoni Melckzedek Humbe akitoa taarifa ya miradi yote wilayani hapo amesema halmashauri imepokea jumla ya Tsh. Bilioni 5.6 ambapo kati ya hizo Tsh.7.3 sawa na asilimia 75.9 ya fedha zilizotengwa.

Aidha Humbe  akasema kwamba miradi iliyotekelezwa  ni ukamilishaji wa vyumba vya maabara katika shule za sekondari, uchimbaji wa  visima katika maeneo mbalimbali na utekelezaji wa shughuli za TASAF.

Ziara hiyo inaendelea kesho katika wilaya ya Iramba na Ikungi baada ya leo kufanyika katika wilaya ya Manyoni na Halmashauri ya Itigi huku kikosi kingine kikendeleza na ziara hiyo wilaya ya Mkalama.

Ziara ikiendelea

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.