• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

KAMATI YA USHAURI NA KLINIKI YA SHERIA YAZINDULIWA SINGIDA

Posted on: May 19th, 2025

 Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe.Halima Dendego amezindua rasmi Kamati ya Ushauri wa Kisheria ngazi ya Mkoa na Wilaya na Kliniki ya Sheria bila malipo kwa Wananchi wa Mkoa wa Singida leo tarehe 19 Mei, 2025 katika viwanja vya Stendi ya zamani Manispaa ya Singida.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mgeni Rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Halima Dendego ameipongeza Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kuuchagua Mkoa wa Singida na kuja kuzindua Kamati ya Ushauri wa Kisheria ngazi ya Mkoa na Wilaya kwa kuwa ni fursa kwa wananchi wa Mkoa huo kutatuliwa changamoto mbalimbali za kisheria zinazowakabili.

"Kipekee naishukuru Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Kamati ya Ushauri wa Kisheria ngazi ya Mkoa na Wilaya kwa kunifikiria na kunipa wajibu huu mkubwa wa kuwa Mgeni Rasmi katika Halfa hii ya Uzinduzi wa Kamati na Kliniki ya Sheria bila malipo katika mkoa wetu”.Amesema Mhe. Dendego.

Mhe. Dendego amesema kuwa kuzinduliwa kwa Kamati hiyo pamoja na masuala mengine, kutasaidia Kupunguza mashauri au migogoro dhidi ya Serikali, kuwawezesha Mawakili wa Serikali kusimamia Utawala wa Sheria katika maeneo yao, Kuwawezesha Mawakili wa Serikali kushirikiana na wadau wengine katika kutatua kero za wananchi na kupunguza malalamiko ya kisheria kutoka kwa wananchi.

“Naomba kukuahidi Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwa nitazisimamia Kamati hizi kikamilifu ili ziweze kuwa na tija katika mkoa wetu.” Amesema Mhe. Dendego

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Singida ametoa wito kwa Wananchi wa Mkoa huo kujitokeza kwa wingi katika Kliniki ya Sheria bila malipo ili waweze kupata huduma mbalimbali za kisheria hususani katika masuala ya mirathi, Ardhi, ndoa na Ajira.

"Nitoe wito kwa Wananchi wa Singida kujitokeza kwa wingi katika Kliniki hii kwani Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imekuja na Wataalamu waliobobea katika masuala ya Kisheria na wanatoa huduma hii bure kabisa.”Amesema Mhe. Dendego

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza S. Johari amesema kuwa kuzinduliwa kwa Kamati ya Ushauri wa Kisheria ngazi ya Mkoa na Wilaya pamoja na Kliniki ya Sheria kwa Wananchi wa Mkoa wa Singida ni mojawapo ya hatua za Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika kusogeza huduma za kisheria karibu zaidi na wananchi.

Aidha, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ameeleza kuwa moja ya njia inayotumiwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwajibika kwa wananchi ni kutoa ushauri na msaada wa kisheria kwa wananchi kwa kutumia Kamati za Ushauri wa Kisheria kwa ngazi ya Mkoa na ngazi za Wilaya.

"Lengo kuu la uanzishwaji wa Kamati za Ushauri wa Kisheria kwa ngazi ya Mkoa na Wilaya ni kurahisisha usimamizi wa utoaji wa ushauri wa kisheria kwa wananchi katika maeneo husika”. Amesema Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

 Uzinduzi wa Kamati ya Ushauri wa Kisheria kwa Mkoa wa Singida utafuatiwa na Kliniki ya sheria kuanzia tarehe 19 hadi 25 Mei, 2025 ambapo huduma za ushauri wa kisheria zitatolewa kwa wananchi bila malipo, ambapo amesisitiza Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali itatoa huduma hizo kwa ubora.

Kliniki hiyo ya Sheria inalenga kusogeza huduma za sheria karibu na wananchi, kuwaongoza wananchi katika taratibu za kupata haki zao pale zinapovunjwa au zinapoonekana kuelekea kuvunjwa, kutoa elimu ya sheria kwa wananchi na kuongeza ushirikiano miongoni mwa Mawakili wa Serikali na Mawakili wa Kujitegemea, na kuepusha au kupunguza mashauri yasiyo ya lazima.




Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • "SINGIDA IMEJIPANGA KUONGOZA UFAULU KITAIFA":RC DENDEGO

    June 04, 2025
  • MRADI WA TACTIC KULETA NEEMA MANISPAA YA SINGIDA.

    June 02, 2025
  • "WAHITIMU MSIBWETEKE,JIENDELEZENI KATIKA FANI ILI MJIAJIRI"-DKT.MGANGA

    May 30, 2025
  • DKT.MGANGA:"WATUMISHI MSIKUBALI KUTUMIKA VIBAYA,KUWENI NA UTAMBULISHO MZURI"

    May 27, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.