• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

KASI YA UTEKELEZAJI YA MIRADI YA MAJI HALMASHAURI YA ITIGI INARIDHISHA.

Posted on: November 26th, 2017

  Utekelezaji wa miradi ya maji katika Halmashauri ya Itigi umeonekana kuwa wenye kasi inayoridhisha licha ya halmashauri hiyo kuanzishwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita.

Kaimu Kaibu Tawala Mkoa wa Singia Buhacha Baltazari Kichinda ametoa tathmini hiyo wakati wa kikao na wataalamu wa halmashauri hiyo ambapo wamejadili mikakati ya kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji.

Kichinda amesema ofisi ya Mkuu wa Mkoa haina wasiwasi kuhusu halmashauri kutekeleza na kusimamia miradi ya maji huku matarajio yakiwa ni ifikapo Juni 2018, asilimia ya upatikanaji wa maji ipande kutoka asilimia 34 za sasa hadi kufikia lengo la mkoa la asilimia 72.

“Mkurugenzi na Mwenyekiti wa Halmashauri mnaonyesha dhahiri mmejitosa kuwapunguzia wananchi adha ya kutafuta maji huku wakiacha kwa muda shughuli zao za uzalishaji mali, nina imani mtafikia asilimia 72 hata kabla ya Juni 2018 kwakuwa fedha mnazo na pia mnafanya usimamizi wa karibu wa miradi”, amesisitiza Kichinda.

Ameongeza kuwa Mkoa wa Singida na hata halmashauri ya Itigi haina mito inayotiririsha maji mwaka mzima hivyo kusababisha uhaba wa upatikanaji wa maji katika kipindi cha kiangazi huku wananachi wakitegemea mabwawa na visima ambavyo vinatakiwa kujengwa na serikali.

“Kipidi cha Kiangazi kwakweli utawahurumia wananchi wanavyosumbuka kutafuta maji, wanatumia muda mwingi huko na kujikuta wana muda kidogo wa kuzalisha mali, hali hii haipendezi na nina imani pia viongozi wa Itigi hili haliwapendezi ndio maana mmeweka nia ya dhati kulitatua ili wananchi wapate muda mwingi wa kuzalisha kwaajili ya maendeleo ya Mkoa na taifa letu”, amefafanua Kichinda.

Naye Mhandisi wa Maji Mkoa wa Singida Lydia Joseph amesema endapo halmahauri hiyo itasimamia kwa umakini na haraka kukamilika kwa miradi ya Itigi mijini, Kitaraka na Aghondi itasaidia ongezeko la upatikanaji wa maji kwa asilimia 20.

Kwa upande wake Mhandisi wa Maji wa Halmashauri ya Itigi Evaristo Mgaya amesema halmashauri hiyo inatekeleza miradi ya maji katika vijiji vya Rungwa, Ipande, Sanjaranda, Itigi, Kitaraka na Aghondi huku kukiwa na mradi wa visima 16 vya ‘windmill’ katika vijiji 12.

Mgaya ameeleza kuwa miradi hiyo itakamilika ndani ya kipindi cha mwaka huu wa fedha yaani kabla ya Juni 2018 hivyo kuongeza upatikanaji wa maji kwa zaidi ya asilimia 72.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Itigi Luhende Pius Shija amesema wamewajibika sana kuboresha upatikanaji wa huduma za maji ambazo ni muhimu katika kukuza uchumi.

Luhende amesema licha ya kuendelea kutekeleza miradi iliyoko kwenye bajeti pia yeye na wataalamu wa idara ya maji wameongeza jitihada kwa  kuwasilisha maombi mengine ya kuonezewa fedha za miradi ya maji ambapo tayari wamekubaliwa hali itayaongeza zaidi upatikanaji wa maji.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.