Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoani Singida leo Februari 11,2025 wametoa elimu kwa viongozi wa dini mbalimbali, viongozi wa kimila,wazee maarufu,viongozi wa asasi zisizo za kiserikali na watu wenye mahitaji maalumu juu ya madhara ya rushwa kuelekea katika Uchaguzi Mkuu 2025,mafunzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi(NAO)mkoani Singida.
Awali akiwasilisha mada katika semina hiyo,Afisa Mwandamizi wa TAKUKURU mkoani Singida, Bw.Joseph John Kailanya ametoa mada kuhusu aina za rushwa katika uchaguzi,makosa ya jinai katika katika uchaguzi na njia mbali mbali za kuripoti taarifa za vitendo vya rushwa na madhara ya rushwa.
"Baadhi ya makosa ya jinai katika uchaguzi ni pale mgombea alijitoa katika kinyang'anyiro cha uchaguzi kwa kupewa rushwa,kuandaa makundi ya kufanya vurugu wakati wa uchaguzi,Mpigakura kumpatia mtu mwingine kadi ya mpiga kura ili kuitumia na kutoa shukurani kwa wapiga kura baada ya uchaguzi kufanyika"amesema Bw.Joseph Kailanya.
Naye Mkuu wa TAKUKURU mkoani Singida Bi.Sipha Mwanjala akizungumza katika semina hiyo ameainisha majukumu ya Taasisi hiyo ambayo ni "KUZUIA NA KUPAMBANA"na rushwa kwa lengo la kuhakikisha haki inatendeka kwa kila mmoja.Pia amewasisitiza wananchi kutumia jukwaa la 'TAKUKURU RAFIKI' ili kupata elimu kuhusu Masula ya rushwa na pia kuwawezesha kuibua kero mbalimbali na kupendekeza namna gani ya kuzitatua.
Pia amewaasa viongozi wa dini kwenda kuelimisha waumini wao kuhusu suala la rushwa kama kosa la kijani na adui mkubwa sana wa kupata viongozi bora na waleta maendeleo.
Akitoa maoni katika semina hiyo,Chifu Mazoya ameomba taasisi hiyo kupeleka elimu hiyo ya rushwa katika makundi na sehemu mbalimbali ili watubwafahamu zaidi kazi zao na kuwafahamisha tofauti ya taasisi hiyo na Askari wa Polisi kwa madai kubwa wananchi wanachanganya majukumu ya taasisi hiyo na yale yanayofanywa na Askari wa Polisi.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe.Halima Dendego ambaye alikua mgeni rasmi katika semina hiyo amezungumzia kuhusu madhara ya rushwa katika uchaguzi akiainisha baadhi ya madhara yake hasi ikiwemo kuchagua viongozi wasiofaa katika jamii ambao hushindwa kuwahudumia wananchi kwa ufanisi pamoja na kuharibu misingi ya demokrasia ambayo hupelekea kuharibu amani na uchumi wa jamii na nchi yetu kwa ujumla.
"Tunao wajibu wa kutoa elimu na kuhamasisha jamii kuiepuka rushwa hususani katika kipindi kijacho cha uchaguzi,ili kuwapata viongozi bora ni lazima tuikemee rushwa ili kudumisha haki na uwajibikaji wao kwa wananchi"amesema Mhe.Dendego.
Pia ameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa TAKUKURU kwa wakati wowote watakapohitaji ushirikiano wao,pia kuwa bega kwa bega katika kuhakikisha vitendo vya rushwa vinatosha kwa lengo la kuhakikisha utendaji bora wa kazi na kwa haki kwa kuhakikisha wote watakaohusika katika vitendo hivyo wanachukuliwa hatua za kisheria.
SINGIDA
Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA
Telephone: 2502170, 2502089
Mobile: 2502170, 2502089
Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz
Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.