• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

KUKU FESTIVAL MEI MOSI SINGIDA MAANDALIZI YAMEKAMILIKA

Posted on: April 2nd, 2025

Mkuu  wa Mkoa wa Singida Mheshimiwa Halima Dendego, amewataka wafanyabiashara wanaochoma nyama ya kuku mjini Singida kujipanga kwa ajili ya kutoa huduma hiyo vizuri kwa mamia ya wageni ambao watakuja  kuhudhuria maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Dunia (Mei Mosi) ambayo yatafanyika kitaifa mkoani hapa.

Alitoa agizo hilo baada ya kufanya ziara ya kushtukiza saa 3:00 usiku akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Singida, Mheshimiwa Godwin Gondwe, Meya wa Manispaa ya Singida Mhe.Yagi Kiaratu, Katibu Tawala Wilaya ya Singida, Bi.Naima Chondo katika eneo la Ubungo Singida mjini ambalo ni maalum kwa ajili ya wafanyabiashara wanaofanya biashara ya kuchoma nyama ya kuku kwa saa 24.

"Tumekuja kuwatembelea hapa kuona hali ilivyo hapa ili wageni wetu watakaokuja kwa ajili ya Mei Mosi wasijisikie vibaya, tunategemea zaidi ya wageni 6000 katika mjini wetu wa Singida na wote wataishi hapa Manispaa ya huduma zote wanategemea kuzipata hapa hapa,"alisema.

Mhe.Dendego amesema kutokana na ugeni huo mkubwa kila mfanyabiashara ajipange kwa kuhakikisha anatoa huduma nzuri na katika mazingira safi ili hata watakapokuwa wameondoka wasimulia jinsi kuku wa Singida walivyo wazuri na watamu.

Naye Meya wa Manispaa wa Singida, Yagi Kiaratu, alishukru kwa mkoa wa Singida kupewa heshima ya kuwa mwenyeji wa siku ya Mei Mosi kwani hali hii itaweza kuongeza kipato kwa wananchi wa Manispaa ya Singida ambao watatumia fursa hiyo kufanya biashara mbalimbali.

"Singida ni mkoa ambao vyakula vya asili vinapatikana, hapa wageni wetu wakija watakula kuku wa asili, ng'ombe wa asili wageni watafurahia vyakula vizuri na vitamu na sisi tumejipanga kutoa huduma kwa kukesha hadi asubuhi," alisema.

Naye Katibu wa Wafanyabiashara Wachoma Kuku eneo la Ubungo, Joseph Raphael, aliishukru serikali kwa kuileta Mei Mosi kitaifa Singida na kwamba wamejipanga kutoa huduma nzuri za nyama ya kuku.

Alisema changamoto zilizopo katika eneo hilo watahakikisha wanazimaliza ili wageni wakija waweze kupata huduma nzuri za chakula na kwamba kwa sasa wameanza kutumia nishati safi ya gesi ili kuweza kuwahudumia kwa uharaka zaidi.

Kabla ya kilele cha maadhimisho ya Mei Mosi shughuli mbalimbali zitafanyika kama vile michezo,utalii wa barabarani lengo likiwa kuwaonyesha wageni wataofika Singida wajue Singida kuna utalii gani.

Sambamba na maandalizi hayo,Mei Mosi Mkoani Singida linatarajiwa kuwa na usiku wa Kuku ( kuku festival), mashindano ya magari, ngoma za asili, makongamano na bonanza la michezo litakaloanza wiki mbili kabla ya kilele cha Mei Mosi.


               "KARIBU SINGIDA-MEI MOSI 2025.' 

                          SINGIDA NI SALAMA

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.