• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

MAADHIMISHO SIKU YA WANAWAKE KUWEKA HISTORIA MKOANI SINGIDA

Posted on: March 1st, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Halima Dendego amesema kuelekea siku ya Mwanamke duniani kimkoa,wameazimia kufanya matendo ya huruma kwa kutembelea na kutoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalumu katika Chuo cha Maendeleo ya Wananchi FDC .

Mhe.Dendego amesema hayo leo ofisini kwake wakati akizungumzia maandalizi ya siku ya Mwanamke kimkoa ambayo yatafanyika tarehe 7/3/2025 katika uwanja wa Bombadia.

Akitoa ratiba ya matukio mbalimbali yatakayofanyika kuelekea kilele cha maadhimisho,Mkuu wa Mkoa amesema kuwa kuanzia leo tarehe Mosi,maadhimisho yameanza katika ngazi ya Vijiji, Kitongoji ,Mitaa,Kata, Tarafa na Halmashauri na kuanzia tarehe 5 Machi, maadhimisho yataanza kufanyika katika ngazi ya Mkoa ambapo shughuli mbalimbali zitafanyika.

Katika Bonanza la Machi 5, kutakuwa na michezo mbalimbali katika uwanja wa Bombadia ikiwemo mpira wa Pete, Ngoma za asili, Muziki wa kizazi kipya, lengo la burudani hizi ni uhakikisha ujumbe wa siku ya Mwanamke kwa mwaka huu unafika kwa umma .

lakini pia tarehe 6/3/2025 kutakuwa na kongamano la wanawake wote kutoka maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Singida kuanzia ngazi ya kijiji mpaka Mkoa na jumla ya wanawake zaidi ya elfu moja(1000) watakuwepo katika kongamano hilo likisindikizwa na Mada Mbalimbali ambazo zitafundishwa na kujadiliwa kama vile Mwanamke na Uchumi, Nishati safi ya kupikia ,mashaka ya ukatili,Mwanamke na Kodi na uwezeshwaji wa Mwanamke kuwa Mama bora.

Tarehe 7/3/2025 itakuwa ndio kilele cha siku ya Mwanamke kimkoa wa ambapo sherehe hizo zitafanyika katika uwanja wa Bombadia zikitanguliwa na maandamano ya Wanawake wote,Burudani mbalimbali na zoezi la utoaji wa tuzo kwa Wanawake waliofanya vizuri katika maswala mbalimbali yanayogusa jamii.

Katika hatua nyingine kueekea mwanzo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, Mkuu wa Mkoa wa Singida amewaomba wafanyabiashara wasipandishe bei ya bidhaa katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani pamoja na Kwaresma ili wawape nafasi ya waumini kupata unafuu wa kupata mahitaji yao katika kipindi hiki.

Siku ya mwanamke duniani inaadhimishwa tarehe 08/03 ya kila Mwaka na kwa Mwaka huu siku hiyo kitaifa itafanyika Mkoani Arusha, kwa Mkoa wa Singida itaadhimishwa tarehe 07.03.2025 katika uwanja wa Bombadia Manispaa ya Singida na Kauli mbiu ya Mwaka huu ni :

           "WANAWAKE NA WASICHANA 2025:TUIMARISHE HAKI, USAWA NA UWEZESHAJI"

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.