• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

Maadhisho ya miaka 60 ya Uhuru mkoani Singida vijana wafanya Kongamano

Posted on: December 6th, 2021

Vijana wametakiwa kuenzi miaka 60 ya uhuru wa Tanzania bara na miaka 59 ya Jamhuri kwa kuangalia  mabadiliko katika nyanja za uchumi utamaduni na namna ya upatikanaji wa viongozi unavyofanyika hapa nchini.

Mkuu wa ya Iramba Suleimani Mwenda akihutubia wakati wa kongamano la vijana katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Manyoni ikiwa ni sehemu ya maadhimisho kimkoa ya miaka 60 ya uhuru wa Tanznaia Bara.

Akiongea katika kongamano la vijana lililofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni,  Mkuu wa ya Iramba Suleimani Mwenda amesema hali ya uchumi wa taifa umebadilika kwa kiasi kikubwa kabla na baada ya uhuru hivyo vijana wanatakiwa kujifunza kutokana na mabadiliko hayo.

DC  Suleimani akabainisha kwamba katika kipindi cha baada ya uhuru kulikuwa na chuo Kikuu kimoja  cha Dar es Salaam ambacho kilichukua wanafunzi wachache hivyo kusababisha waliowengi kukosa fursa ya kupata elimu ya juu, ikilinganishwa na kipindi hiki ambapo vyuo ni vingi.

Amesema ukizungumzia uhuru wa Tanzania unazungumzia uhuru wa nchi nyingi za kiafrika kwakuwa Tanzania ilishiriki katika kutafuta ukombozi wa mataifa mengi ya kiafrika  yakiwemo  Msumbiji, Afrika ya Kusini jambo ambalo vijana wanatakiwa kufahamu hali ya ukarimu ambao umekuwa ni sehemu ya utamaduni wetu. 

Aidha siasa za Tanzania hasa namna ambavyo viongozi wamekuwa wakibadilishwa kwa njia ya chaguzi ambapo mataifa mengi yamekuwa yakishikwa na butwaa hasa kwa kuangalia nchi za jirani na Tanzania ambazo zimekuwa zikiingia kwenye migongano mara kwa mara.

Awali DC huyo alitoa shukrani za dhati kwa wandaaji wa kongamano hilo ambalo linawafungua vijana na kuwafanya kuwa wazalendo na kuwaonesha fursa mbalimbali zinazowazunguka.

DC Mwenda akabainisha umuhimu wa kufanyika kongamano hilo wilayani Manyoni kwa kuwa ilikuwa ni sehemu ya  kuwafundisha vijana umuhimu wa Mashujaa waliotokea Manyoni katika mapambano ya kudai uhuru.

Afisa Vijana Mkoa wa Singida Fredrick Ndahani akizungumza wakati wa kongamano hilo

Kwa upande wake Afisa Vijana Mkoa wa Singida Fredrick Ndahani akaishukuru Serikali kwa kufufua na kuendeleza shirika la ndege nchini na ambapo  awali lilikuwa na ndege moja  lakini  baada ya miak 60 ya uhuru shirika lina ndege 11.

Ndahani alisema shirika hilo linatoa fursa kwa vijana kufanya biashara ndani na nje ya nchi kwa kwa kuwa miundombinu ya barabara  na anga vimeendelezwa kwa kiasi kizuri.

Bwana Ndahani akafafanua kwamba ni jukumu la vijana kulinda miundombinu ya barabara na reli kwa kuwa ndio vitu ambavyo vitawakomboa vijina katika mpango wa usafirishaji wa bidhaa kutoka sehemu moja na kwenda nyingine.

Afisa Vijana huyo akamalizia kwa kusema kwamba mkoa wa Singida unajivunia kuwa na shule nyingi za Sekondari na Msingi ambapo hakuna kijana ambaye ataweza kufaulu akakosa shule alifafanua Ndahani.

Kongamano hilo lilihusisha vijana wajasiriamali, wanafunzi wa shule mbalimbali za wilayani hapo, Maafisa wa Serikali pamoja na umoja wa vijana wa chama cha Mapindizi CCM.

MATUKIO KATIKA PICHA

Vijana wakifuatilia kongamano hilo

Elimu ya Afya ikitolewa wakati wa kongamano hilo


Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.