• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

MADAKTARI BINGWA WAWASILI SINGIDA KUTOA HUDUMA BORA KWA WANANCHI

Posted on: October 6th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Fatuma Mganga, amewataka Madaktari Bingwa waliowasili mkoani humo kuhakikisha wanatoa huduma bora, zenye heshima na utu kwa wananchi ili kuenzi taaluma yao na kuacha alama chanya katika jamii.

Akizungumza leo Oktoba 6, 2025, wakati akiwakaribisha Madaktari Bingwa wa magonjwa mbalimbali maarufu kama Madaktari wa Mama Samia, Dkt. Mganga amesema madaktari hao wamewasili Singida kwa ajili ya kutoa huduma za kibingwa katika Halmashauri zote saba za Mkoa huo kwa muda wa siku tano.

Amesema ni wajibu wa kila daktari kutumia ujuzi wake ipasavyo kwa moyo wa kujituma, upendo na ukarimu ili huduma watakazozitoa ziwe chachu ya matumaini kwa wananchi na kuacha kumbukumbu njema ya kazi yao.

 “Tumetumwa kufanya kazi hii, hivyo yatupasa tukatumike kwa bidii, upendo na ukarimu kama fursa ya kuleta kicheko na baraka kwa wananchi tunaokwenda kuwahudumia,” alisema Dkt. Mganga.

Ameongeza kuwa utoaji wa huduma bora ni wajibu wa kitaaluma unaopaswa kuambatana na ubinadamu na moyo wa kujitolea, hasa kwa madaktari bingwa wanaokwenda kugusa maisha ya wananchi moja kwa moja. Kadhalika, ametoa wito kwa madaktari hao kuonyesha ubingwa wao kwa vitendo kwa kutoa huduma za ubora wa hali ya juu zinazolenga kupunguza idadi ya vifo vya akina mama na watoto, hususan wale waliokuwa wakisafiri umbali mrefu kufuata huduma hizo katika hospitali kubwa za kitaifa kama Muhimbili.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Victorina Ludovick, amewahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi katika vituo vya kutolea huduma hizo za kibingwa ambazo sasa zimesogezwa karibu na maeneo yao.

“Huduma hizi ni za kipekee sana. Wapo wananchi wengi waliokuwa wakisafiri hadi Muhimbili au Bugando kwa ajili ya huduma kama hizi, sasa zimeletwa mlangoni mwao. Ni nafasi ya kipekee ambayo kila mwananchi anapaswa kuitumia,” alisema Dkt. Ludovick.

Ameeleza kuwa huduma zitakazotolewa ni pamoja na magonjwa ya wanawake, watoto, upasuaji, meno na kinywa, magonjwa ya ganzi na usingizi, pamoja na uvimbe, huku zaidi ya wananchi 5,000 wakitarajiwa kufikiwa katika awamu hii.

Mmoja wa Madaktari Bingwa waliowasili mkoani humo alisema kuwa timu yao imejiandaa kikamilifu kuhakikisha wananchi wa Singida wanapata huduma bora na za kibingwa kwa viwango vya juu.

“Tumewezeshwa vizuri na Serikali – tuna vifaa vya kisasa, dawa muhimu na timu kamili ya wataalamu wa fani mbalimbali. Tumejipanga kutoa huduma bora, zenye matokeo chanya kwa wananchi,” alisema mmoja wa madaktari hao.

Ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuimarisha sekta ya afya kupitia mpango huu wa Madaktari Bingwa unaolenga kufikisha huduma bora kwa wananchi katika ngazi za mikoa na halmashauri.

Uwepo wa Madaktari Bingwa mkoani Singida unatarajiwa kuleta manufaa makubwa kwa wananchi, ikiwemo kupunguza gharama za kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za kibingwa, kuimarisha afya ya jamii kwa kugundua na kutibu magonjwa mapema, kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu afya kupitia elimu itakayotolewa sambamba na huduma, pamoja na kuongeza ujuzi kwa watumishi wa afya wa mikoa na halmashauri kupitia mafunzo ya vitendo kutoka kwa madaktari hao.

Huduma hizo za kibingwa zitaendelea kutolewa kwa muda wa siku tano katika vituo maalum vilivyopangwa kwenye halmashauri zote saba za Mkoa wa Singida, zikilenga kuboresha afya ya wananchi na kuunga mkono juhudi za Serikali katika kusogeza huduma bora za afya karibu na wananchi wote.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • MAAFISA UGANI WAASWA KUWA WATATUZI KERO ZA WAKULIMA SHAMBANI

    February 02, 2026
  • TSH. 27,000/- PEKEE KUWASHA UMEME KILA KAYA.

    February 03, 2026
  • SINGIDA YAWEKA MKAZO KILIMO CHA ALIZETI NA MALEZI BORA KWA WATOTO

    February 01, 2026
  • "KILA MMOJA ALINDE ENEO LAKE NA KUFUATA SHERIA" - RC DENDEGO

    January 27, 2026
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.