• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2024 ZAZINDUA UJENZI WA MRADI WA MAJI MABONDENI ITIGI

Posted on: July 6th, 2024

KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2024 , Godfrey Mnzava, ameiagiza Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijiji (RUWASA) kuweka utaratibu wa kuziwezesha Jumuiya za Watumia Maji kifedha na mafunzo ili ziweze kutunza vizuri raslimali maji na miundombinu na hivyo kudumu muda mrefu kutoa huduma za maji kwa wananchi kwa kiwango bora.

Ametoa agizo hilo leo (Julai 6, 2024) wakati wa kuzindua mradi wa maji katika kijiji cha Mabondeni Halmashauri ya Itigi wilayani Manyoni Mkoani Singida ambao umegharimu Sh.milioni 280 ambao utahudumia zaidi ya wananchi 2500.

Mnzava amesema serikali imekuwa ikitoa fedha nyingi kwa ajili ya kujenga miradi ya maji ili kuwawezesha wananchi kupata huduma ya maji safi na salama hivyo miundombinu ya miradi hiyo inatakiwa kutunza vizuri ili iendelee kutoa huduma hizo na jukumu hilo linapaswa kufanywa na Jumuiya za Watumia Maji.

Amesema pia wananchi wanapaswa kutunza vyanzo vya maji visiharibiwe kwani vyanzo vya maji vikiwepo vitaongeza upatikanaji wa maji na hivyo kuondoa kero ya upatikanaji wa maji kwa wananchi kama ilivyo dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muunganow wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kusogeza huduma za maji kwa karibu kwa wananchi.

Aidha, Mnzava ambaye aliridhia mradi huo na kuuzindua ameipongeza RUWASA kwa kutekeleza vyema mifumo ya manunuzi ya umma hali ambayo imesaidia kupunguza malalamiko kwamba wapo baadhi ya wakandarasi wanapendelewa kupewa zabuni za kujenga miradi ya maji.

Awali Meneja wa RUWASA Wilaya ya Manyoni, Mhandisi Gabriel Ngongi, akitoa taarifa ya mradi huo amesema mradi huo uliibuliwa na wananchi mwaka 2022 kwa nia ya kupunguza tatizo la ukosefu wa maji.

Amesema ujenzi wa mradi huo ulianza Agosti 1,2023 na kukamilika Juni 15, 2024 ambapo una kisima chenye uwezo wa kuzalisha maji lita 4,000 kwa saa.

Ngongi amesema ujenzi wa mradi huo ulikadiriwa kutumia kiasi cha Sh. 280,800,000 ikiwa ni fedha kutoka Serikali kuu kupitia Programu ya malipo kwa Matokeo (P4R) lakini hadi kukamilika mradi umetumia kiasi cha Sh. 275,880,099.72.

Amesema fedha hizo zimetumika kujenga Pump House, uunganishaji Mfumo wa umeme, kununua na kufunga mitambo ya kusukuma maji, ujenzi wa mtandao wa bomba, ujenzi wa Tenki la maji la lita 54,000 kwenye mnara wa meta 12 pamoja na Ujenzi wa vituo 5 vya kutolea huduma ya maji.

Meneja huyo amesema faida za mradi huo ni pamoja na kuboresha kipato cha wananchi kwa kutumia muda mfupi wa kupata maji safi na salama kwa gharama nafuu na hivyo kutumia muda mwingi uliobakia kwenye shughuli za uzalishaji, kuboresha afya za wakazi wa kijiji cha Mabondeni.

Faida nyingine ni kujenga mazingira mazuri ya wanafunzi kujisomea badala ya kutumia muda mwingi kutafuta maji atokapo shuleni na kupungua kwa kero kwa viongozi itokanayo na Malalamiko ya kila siku ya ukosefu wa maji safi na salama.

"Sisi Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, hususani Kijiji ya Mabondeni kwa heshima kubwa tunamshukuru sana Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutuletea fedha kwa ajili ya ujenzi wa mradi huu. Tumeona nia ya dhati ya Serikali Kumtua mama ndoo ya maji kichwani na tunaahidi kutunza mradi huu ili uendelee kuinufaisha jamii na kwa maendeleo endelevu".



Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.