• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

MKOA WA SINGIDA WAANZA KUTOA CHANJO YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI KWA WASICHANA 178,114.

Posted on: April 22nd, 2024

Mkoa wa Singida umezindua rasmi zoezi la utoaji wa chanjo wa Saratani la mlango wa kizazi kwa wasichana mwenye umri kati ya miaka Tisa (9) hadi 14 ambapo Wasichana 178, 114 wanatarajiwa kupatiwa chanjo hiyo mkoani humo.

Akizindua zoezi la utoaji wa Chanjo hiyo katika Kijiji cha Kisaki Manispaa ya Singida, Mkuu wa mkoa wa Singida Mheshimiwa Halima Dendego (leo 22-Aprili-2024 ) amewaagiza Maafisa Afya wahakikishe maeneo yote yaliyoandaliwa kutolewa huduma hiyo ya chanjo yanafanya hivyo kwa viwango vya juu ili kuwalinda watoto wa kike na saratani hiyo hatari.

Dendego amesisitiza kuwa chanjo hiyo pia ni lazima iwafikie wanafunzi wanaosoma kwenye shule binafsi na watoto wa kike ambao wanaishi mitaani nao wapate fursa ya kupata chanjo hiyo ili kuwakinga na saratari na mlango wa kizazi.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Halima Dendego, akizungumza kwenye uzinduzi wa zoezi la utoaji wa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi iliyofanyika kimkoa katika Shule ya Msingi Kisaki Halmashauri ya Manispaa ya Singida.

“Tunapoenda kuwalinda watoto wa kike kwa kuwachanja chanjo hiyo maana yake tunawaepusha na madhara ugonjwa wa saratani ili wasije wakaambukiza wavulana”Ameeleza RC. Halima Dendego.

Amesisitiza kuwa chanjo hiyo ni muhimu kwa wasichana na inatolewa bure kwa sababu Serikali kwa kushirikiana na Wadau wa maendeleo imegharamia chanjo hiyo, hivyo ni muhimu kwa wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao kupata chanjo hiyo ili kuwaepusha na madhara yanayoweza kutokea. 

Kwaupande wake, Mganga Mkuu mkoa wa Singida Dkt. Victorina Ludovick amesema kwa Tanzania chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi (HPV) ilianza majaribio mwaka 2014 mkoani Kilimanjaro na kupata mafanikio makubwa kwa kuwakinga wasichana wasipate ugonjwa huo.

Dkt. Victorina Ludovick ameeleza mtu yeyote anaweza kuambukizwa saratani hiyo katika umri wowote ule hasa wakati wa tendo la ndoa na inaweza kusababisha magonjwa mengine ikiwemo saratani ya koo na magonjwa mengine ya via vya kizazi kwa wanamke na wanaume.

Naye, Katibu Tawala wa mkoa wa Singida Dkt. Fatuma Mganga amewataka Maafisa Afya wanaotoa chanjo hiyo kuhakikisha wanafanikisha zoezi hilo kwa viwango ili mkoa wa Singida uwe wa kwanza katika utoaji wa chanjo hiyo kwa wasichana mwenye umri wa miaka Tisa hadi 14.  

Amesema saratani hiyo inaua na ni ugonjwa hatari hivyo ni muhimu kwa watoto wote wenye umri wa kupata chanjo wapewe kutokana na umuhimu wake katika kulinda afya zao.

Nao, Mashuhuda waliopewa chanjo hiyo wakizungumza kwenye uzinduzi wa utoaji wa chanjo ya satarani la mlango wa kizazi katika kijiji cha Kisaki Manispaa ya Singida Lukuresia Andrea na Salisabila Athumani wote wakazi wa mkoa wa Singida wamesema tangu wapatiwe chanjo hiyo hawajapata madhara yoyote hivyo wameomba wazazi na walezi wasiwazuie watoto wao wa kike kwenda kupata chanjo hiyo kwa sababu inafaida kubwa katika maisha yao.

Katibu Tawala wa mkoa wa Singida Dkt. Fatuma Mganga akizungumza kwenye uzinduzi wa zoezi la utoaji wa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi.

Zoezi la kuimarisha chanjo ya HPV litakamilika tarehe 26 Aprili, 2024 hata hivyo hudumaa hiyo itaendelea kutolewa kwa utaratibu wa zamani yaani shuleni, vituo vya kutolea huduma za afya na kwenye huduma za mkoba za Masuala ya Afya ya Uzazi na Mtoto.

Chanjo ya HPV, kama ilivyo kwa chanjo nyingine zinazotolewa kupitia Mpango wa Taifa wa Chanjo, haiuzwi kwa mteja yeyote, hivyo inatolewa bure kwa walengwa katika vituo vyetu vya kutolea huduma.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mheshimiwa Halima Dendego (mwenye koti rangi nyekundu), akiwa na wanawake waliopata chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi mkoani Singida waliokaa na watoto wao, Pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali.

Baadhi ya Wanawake waliopata chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi mkoani Singida wakiwa na watoto wao.








Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.