• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

MKOA WA SINGIDA WAKABIDHI MWENGE WA UHURU KWA KISHINDO. *JUMLA YA MIRADI 42 YENYE THAMANI YA TSH. BILIONI 15.3 IMEKUBALIWA*

Posted on: September 30th, 2023

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Fatuma Mganga kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo Peter Serukamba jana tarehe 29 Septemba, 2023 amekabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Ally Gugu kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo Rosemary Senyamule huku jumla ya miradi ya maendeleo ikiwa ni 42 yenye dhamani ya Tsh Bilioni 15.3 iliyokuwa inapitiwa na Mwenge wa Uhuru imekubaliwa.

Mwenge wa Uhuru ulipokelewa Mkoani Singida tarehe 22 Septemba, 2023 kutoka Mkoani Tabora na kukimbizwa kwa muda wa siku 7 katika Wilaya 5 zenye Halmashauri 7 kwa kuanzia Iramba na kuhitimisha Wilayani Manyoni kwa lengo la kufikisha ujumbe wa Mwenge wa Uhuru 2023 ukikagua miradi ya ujenzi nyaraka za manunuzi kuweka jiwe la msingi kufanya uzinduzi ambapo imeelezwa miradi yote imetekelezwa kwa viwango.

Aidha Wananchi wa Mkoa wa Singida wamepokea vema ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023 ambao umetolewa maeneo mbalimbali ya Halmashauri za Mkoa huo ambao ni “Tunza Mazingira, Okoa Vyanzo vya Maji kwa Ustawi wa Viumbe Hai kwa Uchumi wa Taifa”.

Hata hivyo Dkt. Fatuma Mganga amemshukuru na kumpongeza Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2023, Abdalla Shaib Kaim pamoja na wenzake wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa kuleta ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu kwa umahiri mkubwa.

“Wananchi wa Mkoa wa Singida kwa pamoja kupitia ujumbe huo mwambatano wa Mwenge wa Uhuru tumejifunza kuhusu : -

Mapambano dhidi ya Rushwa, chini ya Kauli mbiu “Kuzuia Rushwa ni Jukumu Lako na Langu: Tutimize Wajibu Wetu”.

Mapambano dhidi ya Malaria, chini ya kauli mbiu “Ziro Malaria Inaanza na Mimi – Nachukuahatua kuitokomeza”.

Mapambano dhidi ya Dawa za kulevya, chini ya kauli mbiu “Tukabiliane na Changamoto za Dawa za Kulevya wakati Wote kwa Ustawi wa Jamii”.

Mapambano dhidi ya VVU / UKIMWI chini ya kauli mbiu “Imarisha Usawa, Tokomeza Ukatiliwa Kijinsiana Unyanyapaa”.

Lishe Bora kwa afya imara, chini ya kauli mbiu “Lishe ni Msingi wa Maendeleo Sote Tuwajibike”. Dkt. Fatuma Mganga

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Abdalla Shaib Kaim, ameeleza kuwa miradi yote iliyotembelewa katika Mkoa wa Singida na Halmashauri zake imeonekana kutekelezwa kwa kiwango kinachotakiwa na Serikali. Aidha amewasisitiza Wakurugenzi na Wakuu Wilaya kuhakikisha wanafanyia kazi ushauri na maelekezo yaliyotolewa kwa baadhi ya miradi kwa ajili ya kuboresha zaidi.

Sambamba na hilo Kaim ameelekeza kwa watendaji wa halmashauri zote nchini kuhakikisha wanasimamia miradi yote ya maendeleo na kuikamilisha kwa wakati ili iweze kutumika kama ilivyo kusudiwa.

Katika mbio hizo za Mwenge wa Uhuru miradi mbalimbali ilionekana kuwagusa zaidi wananchi katika Mkoa wa Singida ambapo ni utekelezaji wa miradi ya barabara, miradi ya maji, sekta ya Elimu, Sekta ya Afya pamoja na miradi mbalimbali ya vijana.

Pamoja na mambo mengine wananchi wameeleza kuwa miradi iliyozinduliwa na kuwekewa jiwe la msingi ni miradi muhimu kwa maendeleo ya wananchi na itasaidia kupunguza kero ambazo zilikuwa zikionekama kuwa sugu.

Baadhi ya wananchi wamesema miradi ambayo inahusika na sekta ya maji itasaidia kupunguza adha waliyokuwa wakiipata wakina mama kutembea umbali mrefu kufuata maji pamoja na kuwapa uhakika wa kupata maji safi na salama.

Wananchi hao kwa nyakati tofauti wameeleza kuwa ujenzi wa vituo vya Afya na Zahanati pamoja na ugawaji wa vyandarua kwa akina mama wajawazito na watoto chini ya miaka mitano itasaidia kupunguza maambukizi ya vimelea vya ugonjwa wa Malaria pamoja na kupunguza vifo vya mama wajawazito na watoto kwa kuwa huduma hiyo imewasogelea wananchi.

Hiyo kama haitoshi wameeleza kuwa uwepo wa barabara za uhakika zilizowekewa jiwe la msingi zitachochea maendeleo kwa maana zitafanya watu kutumia muda sahihi hususani kwa wafanya biashara.


Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.