• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

NAIBU WAZIRI MKUU APONGEZA PAREDI YA MIFUGO KWENYE MAONESHO YA KIMATAIFA YA NANE NANE JIJINI DODOMA.

Posted on: August 5th, 2024

Naibu Waziri Mkuu Mhe. Dotto Biteko, amewaagiza Maafisa ugani kote nchini kuhakikisha wanatoa elimu bora na stahiki kwa Wafugaji, Wakulima na Wavuvi kama hatua ya kuongeza tija ya uzalishaji katika sekta hizo kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya masoko ya ndani na la Kimataifa.

Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Nishati ametoa kauli hiyo katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa mkoa wa Singida Mheshimiwa Halima Dendego, (5 Agosti, 2024 ) katika ufunguzi wa mashindano ya paredi ya mifugo mbalimbali katika Maonesho ya Kimataifa ya Nane nane yanayofanyika katika Viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma.

Ameeleza kuwa paredi ya mifugo huchangia kuhamasisha, kukuza na kuendeleza ufugaji bora katika kuchangia katika maendeleo ya Taifa na mtu mmoja mmoja.

 

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mheshimiwa Halima Dendego, akizungumza kwa niaba ya Naibu Waziri Mkuu Dotto Biteko, katika ufunguzi wa mashindano ya paredi ya mifugo mbalimbali katika Maonesho ya Kimataifa ya Nane nane yanayofanyika katika Viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma.

“Mifugo ni utajiri fugeni kisasa mtaona matunda yake haraka,” Amesisitiza Biteko 

Amesema ufugaji wenye tija kwa kutumia teknolojia na mbinu za kisasa utasaidia kwa kiasi kikubwa wananchi hasa wafugaji, wakulima na wavuvi kuongeza vipato maradufu na kuchangia pato la taifa kwa kiwango kikubwa.

Biteko ameeleza kuwa mafanikio hayo yatafikiwa iwapo tu Maafisa Ugani kote nchini watawajibika ipasavyo katika utoaji wa elimu ya ufugaji wa kibiashara utakaosaidia kukidhi mahitaji ya masoko ya ndani na nje ya nchi.

Kwa upande wao, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Alexander Mnyeti na Naibu Waziri wa Kilimo David Silinde, wamewahakikishia wananchi kuwa Serikali inaendelea kuweka mipango na mikakati madhubuti ili kuhakikisha sekta hizo zinaongeza tija katika uzalishaji kama hatua ya kuwaondoa wananchi na umaskini wa kipato.

Mashindano ya Paredi ya Mifugo yamekuwa kivutia kikubwa kwa wananchi kwa sababu hujumuisha mifugo bora yenye umri mdogo kati ya miaka Mitatu hadi Minne ambayo imefugwa kisasa kwa kuwa na kilo kati ya 700 hadi 800 pamoja na ng’ombe wanaotoa maziwa mengi.

Kwa sasa Tanzania inakadiriwa kuwa na zaidi ya ng’ombe Milioni 37, Mbuzi Milioni 27.6, Kondoo Milioni 9.4 na Kuku Milioni 103.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.