• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

Ofisi za Shule Bora zafunguliwa rasmi Mkoani Singida.

Posted on: November 28th, 2022

Mkoa wa Singida umesema mikakati mbalimbali ya kuboresha ufundishaji na ujifunzaji wa elimu katika shule za Sekondari na Msingi kama sehemu ya ushirikiano na wadau wengine wakiwemo shule bora katika kuimarisha elimu kwa watoto wote.

Kauli hiyo imetolewa leo na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Stanslaus Choaji, wakati wa uzinduzi wa Ofisi ya Mradi wa shule bora Mkoa wa Singida ambapo alieleza juhudi za Serikali kwa kushirikiana na wadau hao kuboresha ujifunzaji, ufundishaji na ujumuishi wa elimu ya Msingi na Sekondari.

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Stanslaus Choaji, akizungumza wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa Ofisi hiyo.

Aidha Choaji ameeleza kwamba kwa kutoa eneo la ujenzi wa Ofisi kwa ajili ya mradi huo inadhihirisha uhusiano mzuri uliopo baina ya Serikali ya Mkoa na mradi wa shule bora jambo ambalo ameeleza kwamba linaweza kuleta matunda na kufikiwa kwa malengo ya Serikali na mradi huo.

Hata hivyo Kaimu Katibu Tawala huyo ametoa pongezi kwa timu ya Mradi wa Shule bora kwa namna ambavyo wameanza kutekeleza majukumu yao mbalimbali kupitia Halmashauri za Mkoa huo.

Choaji ameahidi kwa Niaba ya Serikali ya Mkoa kushirikiana na wadau hao kufanikisha mipango waliojiwekea kumkomboa mtoto wa shule ndani ya Singida na Taifa kwa ujumla.

Mkuu wa Kitengo cha huduma ya Jamii Ubalozi wa Uingereza Getrude Mapunda, akizungumza wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa Ofisi hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha huduma ya Jamii Ubalozi wa Uingereza Getrude Mapunda, amesema Mradi hauanzishi vitu vipya zaidi unatekeleza mipango ya Halmashauri ili kuunganisha rasilimali fedha na rasilimali Watu kutoka Serikali na mwenye Mradi ili kuwasaidia watoto wa kitanzania.

"Mradi hauna fedha nyingi kuliko za Serikali hivyo tukichanganya fedha nyingi za Serikali na zile kidogo za Mradi tunaweza kufikia malengo ya Halmashauri zilizojiwekea katika kuboresha Elimu ya Msingi na Sekondari " alisema Getrude.

Hata hivyo ameomba ushirikiano uliopo uendelee baina ya Mkoa wa Singida na shule bora ili kufikia malengo waliyojiwekea huku akibainisha kwamba changamoto za wanafunzi mashuleni zinatofautiana kwa kila Mkoa.

Mratibu wa Mradi wa Shule Bora Mkoani Singida Samweli Daniel, akitoa taarifa wakati wa hafla ya uzinduzi huo.

Awali akitoa taarifa yake kwenye Mkutano huo Mratibu wa Mradi wa Shule Bora Mkoani Singida Samweli Daniel, amewapongeza viongozi wa Shule bora ambao wametokea Ubalozi wa Uingereza kuja kwenye uzinduzi wa Ofisi hiyo.

Amesema uwepo wa Ofisi hizo utasidia sana katika utekelezaji wa majukumu yao hasa kuhakikisha shule bora inaboresha ujifunzaji, ufundishaji, ujumuishaji na uimarishaji wa mifumo ya elimu.

Amesema kupitia Mradi huo watahakikisha changamoto hizo zinazokabili elimu mkoani hapo zinakwisha na watoto wanapata elimu Bora kwa usawa.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • "SINGIDA IMEJIPANGA KUONGOZA UFAULU KITAIFA":RC DENDEGO

    June 04, 2025
  • MRADI WA TACTIC KULETA NEEMA MANISPAA YA SINGIDA.

    June 02, 2025
  • "WAHITIMU MSIBWETEKE,JIENDELEZENI KATIKA FANI ILI MJIAJIRI"-DKT.MGANGA

    May 30, 2025
  • DKT.MGANGA:"WATUMISHI MSIKUBALI KUTUMIKA VIBAYA,KUWENI NA UTAMBULISHO MZURI"

    May 27, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.