• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

RC Mahenge Aagiza Kuundwa Kwa Kamati Ya Usuluhisho Wa Shamba La Mpambaa

Posted on: March 4th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge ameagiza kuundwa kwa Kamati ya wataalamu wa ardhi kutoka halmashauri za Mkalama na Singida Vijijini ili kutatua mgogoro wa shamba la Serikali lililopo katika Kijiji cha Mpambaa lengo likiwa kuondoa adha wanazozipata wananchi wa maeneo hayo.

Dkt. Mahenge ametoa maelekezo hayo Aprili 3, 2022 mara baada ya kukutana na watendaji wa halmashauri hizo katika ukumbi wa mikutano ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo na kusikiliza malalamiko ya pande zote mbili kwa lengo la kupata utatuzi zaidi wa mgogoro unaoendelea.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge akizungumza wakati wa kikao hicho

Akipokea taarifa kutoka pande mbili za mgogoro imeelezwa kwamba umekuwa na uharibifu wa mazao kutokana na kuliwa na mifugo katika mashamba hayo ambayo imekuwa ikisababisha hasara kubwa kwa wakulima.

Wakati huo wafugaji nao wakilalamikia zoezi la ukamataji wa mifugo ambayo mingine ilipigwa mnada baada ya kukamatwa ikiwa inaharibu mazao hayo.

Kutokana na vitendo hivyo RC Mahenge akasisitiza uundwaji wa kamati hiyo kwa haraka na kuhakikisha inatekeleza majukumu yake kwa kuzingatia haki kanuni sheria pia kamati ihakikishe inashirikisha wananchi wa maeneo husika.

Akiendelea kuzungumza katika kikao hicho Dkt. Mahenge akawasisitiza viongozi hao kutokuwa chanzo cha migogoro bali kwenda kuwasihi wananchi wao kuendelea kuwa na uvumilivu wakati serikali inaendelea na taratibu za kitaalamu ambazo zitakamilika kabla ya msimu ujao wa kilimo.

Akimalizia mazungumzo yake Mkuu wa Mkoa huo amesema kwa kuwa msimu huu shughuli za kilimo na kiuchumi zilishaanza katika shamba hilo hivyo ziendelee kama kawaida hadi hapo timu ya wataalamu iliyoundwa itakapokamilisha zoezi lake na kutoa taarifa ndipo tamko rasmi litatolewa na serikali ya Mkoa.

Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskas Muragili akizungumza wakati wa kikao hicho

Awali akielezea mgogoro huo Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskas Muragili aliunga mkono uundwaji wa kamati hiyo ambapo amesema sababu ya mgogoro huo sio wananchi bali ni baadhi ya viongozi pamoja na wataalamu waliohusika na masuala ya upimaji ardhi.

Hata hivyo Dc Muragili alisema Halmashauri ya Singida Dc ilianza kulisimamia shamba hilo takribani miaka 23 kuanzia mwaka 1999 hadi leo 2022.

“Sisi sote ni ndugu, Viongozi tukae na wataalamu ili kuziangalia kwa kina GN zilizotumika kupata mipaka ya maeneo ya pande zote ili tuweze kukubaliana. Swala la mpaka ni tamko tuu hivyo nashauri tutatue kwanza tatizo la GN”. Alisema Mhandisi Muragili

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Sophia Kizigo akizungumza wakati wa kikao hicho

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Sophia Kizigo amesema alipokea historia ya shamba hilo kutoka kwa mwananchi wake anayeishi jirani na shamba hilo ambapo alielezwa kuwa hapo awali shamba hilo lilikuwa likisimamiwa na serikali ya mkoa kwa shughuli za mradi wa uzalishaji mbegu za Mtama, Alizeti, Mahindi na mazao mengine.

Alielezwa kuwa mara baada ya mradi huo kusitishwa baadhi ya wananchi wa kijiji cha jirani na shamba wakaanza kulitumia kwa shughuli za kilimo ili kujikwamua kiuchumi. Baada ya kupokea historia hiyo Mkuu wa Wilaya huyo aliamua kutuma timu ya wataalamu wa ardhi ili kutambua mipaka ya pande hizo ambapo ikabainika changamoto ni vifaa vilivyotumika kutambua mipaka kuwa hazitoi taarifa zinazofanana.

Akizungumza kwenye kikao hicho Sophia Kizigo alisema wananchi wa upande wa Mkalama wanasubiri kusikia tamko la serikali ya Mkoa kuhusu suluhisho la mgogoro huku akisisitiza weledi na utaalamu ufanyike katika zoezi hilo ili kupata utambuzi wa mipaka hiyo kwa usahihi na si kufuata kihistoria.

Kikao hicho kilihitishwa na Mkuu wa Mkoa huo na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dorothy Mwaluko, Wakuu wa Wilaya ya Singida Dc na Mkalama, Wakurugenzi, Wenyeviti wa Halmashauri za wilaya husika, Wabunge, watendaji wa halmashauri ya Singida Dc na Mkalama pamoja na wananchi wanaoishi jirani na shamba hilo.

kikao kikiendelea

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.