• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

RC Mahenge Azitaka Kamati za Ujenzi wa Madarasa Kuimarisha Usimamizi

Posted on: November 23rd, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge leo amefanya ziara ya kushtukiza katika shule sita (6) za Sekondari  katika  Manispaa ya Singida Mjini zinazoendelea na ujenzi wa vyumba vya madarasa kupitia fedha za UVIKO 19 lengo likiwa ni kujionea hatua iliyofikiwa katika  ujenzi huo na kusisitizia ukamilishwaji ndani ya wakati.

Akiwa katika ziara hiyo Dkt. Binilith Mahege  akazitaka kamati za ujenzi wa shule kutumia muda wao mwingi katika usimamizi wa ujenzi huo ili kupata majengo yenye ubora unaokubalika na kukamilika kwa muda maalum.

Aidha Dkt. Mahenge akakemea vikali kitendo cha kamati za ujenzi wa shule kuwaachia kazi ya usimamizi wakuu wa shule ambapo inafahamika wazi kwamba wanamajukumu mengine ya kusimamia nidhamu na masomo kwa ujumla katika shule zao.

Hata hivyo RC akawataka walimu wakuu wanaosimamia ujenzi huo kuhakikisha kila jengo linakamilika katika kipindi kilichopangwa ambacho ni tarehe  1/12/2021, kwa kuwa kila shule imeonekana kuwa na vitendea kazi vya kutosha.

Dkt. Mahenge akatoa maelekezo kwa watendaji wa Mkoa, Wilaya na Halmashauri kuhakikisha kunakuwepo na wasimamizi kwa kila jengo linalojengwa mkoani hapa.

Aidha RC akamkumbusha Mkurugezi wa Manispaa ya Singida Mjini Zefrin Kimolo Lubuva kuwatumia wakuu wa Idara mbalimbali waweze kusimamia ujenzi na ikiwezekena kila Mkuu wa Idara apewe mradi wake alifafanua.

Amebainisha kwamba changamoto nyingi ambazo zimeonekana katika ujenzi unaoendelea katika Manispaa hiyo ni usimamizi mdogo ambao umeachwa kwa wakuu wa shule peke yao hivyo kila Mkuu wa Idara apatiwe shule ya kusimamia mpaka ujenzi ukamilike alibainisha Dkt. Mahenge

Awali Mkuu wa Mkoa alitoa pongezi kwa wakuu wa shule kwa namna ambavyo waliweza kuendelea kusimamia ujenzi huo na kufikia hatua nzuri. Shule zilizotembelewa ni  Chief Senge, Mandewa, Kindai Sekondari, Mitunduruni, Unyambwa na Mnyamikumbi kati ya hizo ni shule mbili ambazo zilikuwa zipo hatua ya msingi wakati nyinge zikiwa katika hatua ya linter na kuezeka.  

      Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhe.Pasikas Muragili akafafanua kwamba tayari wameshaunda timu  maalumu ya ufuatiliaji ambayo tayari imeshaanza kazi ili kusaidia usimamizi wa kazi hiyo.

DC huyo amewakumbusha mafundi na wasimamizi wa majengo hayo kwamba siku saba zilizobaki zikitumiwa vizuri uwezekano wa kumaliza kazi hizo ni mkubwa endapo kila saa litatumika vizuri.

Amewataka wahandisi kuendelea kusimamia kazi hiyo kwa ufanisi mkubwa na kuhakikisha kunakuwepo na mawasiliano ya kila siku kati yao na Mkurugezi wa Halmashauri ili kuweza kutataua changamoto yeyote itakayoweza kujitokeza.

Naya Mkuu wa Shule ya Sekondari Unyambwa  Bwana Charles Mtaturu amesema moja ya changamoto ambayo kwa kiasi kikubwa imekuwa ikitatiza ujenzi huo ni upatikaji wa vifaa vya kazi na mafundi kwa ajili ya ujenzi

Bwana Mtaturu amebainisha kwamba viwanda vingi vilikuwa vimeshachukua Maagizo kwa watu mbalimbali na mafundi wengi wamewahiwa katika kazi nyingine kwa kwawa mainisapaa hiyo shule ujenzi wa mashule unafanyika kila mahali.

Yagi Maulidi Kiaratu ni Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida mjini  akitoa shukrani kwa washiriki wa ziara hiyo amesema ujio wa Mkuu wa Mkoa wa kushtukiza  kutaongeza  chahu na  uhamasishaji   katika kukamilisha kazi hiyo.

Amesema kwa upande wake atashirikiana na  madiwani pamoja na chama Tawala CCM ambapo wataaza rasmi ziara kama hiyo kuanzia kesho tarehe 24/11/2021 kutembelea miradi yote ya ujenzi wa vyumba vya madarasa.

Aidha amemalizia kwa kusema  siku zilizobaki zinaweza kukamilisha shughuli zote za ujenzi endapo kila mdau atafanya kazi yake kwa kuzingatia muda na mikakati iliyowekwa.

Mwisho

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.