• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

RC Serukamba amewataka wakulima waliopewa mashamba kwenye Skimu ya umwagiliaji Itagata kuyaendeleza haraka mashamba hayo.

Posted on: August 11th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amewataka wakulima waliopewa mashamba kwenye Skimu ya umwagiliaji Itagata katika Halmashauri ya wilaya ya Itigi mkoani Singida kuyaendeleza  haraka mashamba hayo kwa kuyalima mazao yenye tija kwa mtu binafsi na Serikali vinginevyo Serikali itawanyang'anya na kuwapa watu wengine.

RC Serukamba amesema hayo baada ya kufanya ziara ya kikazi kukagua shughuli za kilimo zinazofanywa na wakulima kwenye skimu hiyo ambayo imeigharimu Serikali bilioni 2.1 hadi kukamilika kwake.

Akiwa katika mashamba ya wakulima kwenye skimu  ya Umwagiliaji Itagata Itigi RC Serukamba amesikitishwa na kilimo kinavyoendelea ambapo kati ya ekari 209 walizogawiwa wakulima ambao ni wananchama wa umoja wa umwagiliaji Itigi ekari 40 tu ndizo walizolima muda wa kiangazi jambo ambalo amesema halitakubalika.

"Serikali imewekeza fedha nyingi sana kwenye mradi huu na mimi nimefika kwenye mashamba haya nimeyaona, watu wengi hawajalima kuna jumla ya ekari 209 lakini ekari zilizolimwa kiangazi hiki ni 40 tu mashamba na maji yapo, sasa hii haikubaliki lazima watu walime ili kuisaidia Serikali kupata mapato, Tume ya umwagiliaji nao wapate tozo zao" alisema Serukamba

Aidha Mhe. Serukamba ameongeza kwa kuwataka wananchama wote wa ushirikia kuandaa mkutano ambao  utakuja kubainisha na kuwatambua wakulima waliopewa mashamba, na ambapo wanalima kutumia skimu hiyo.

"Mwezi wa tisa mwenyekiti andaa mkutano na wanachama wako ili tuje tujue nani analima na nani halimi ili wale ambao hawalimi tuwaondolee mashamba tuwape wengine ambao watalima na kuipa Serikali mapato pamoja na Tume ya umwagiliaji" Aliongeza Mkuu huyo wa Mkoa Singida

Mkuu huyo wa Mkoa alisisitiza kuwa faida atakayoipata mkulima kupitia kilimo kwenye skimu hiyo itamrahishia maisha kiuchumi ataweza kuhudumia familia, kulipa bima ya afya  pamoja na kuchangia maendeleo ya taifa lake.

Akizungumza mbele ya Mkuu wa Mkoa mkulima anayejulikana kama Chacha Marwa alisema kuwa changamoto mojawapo inayopelekea  wakulima wengi kutolima ni kushindwa kutambua aina ya udongo  pamoja na baadhi ya Wanachama  wa umoja huo wa umwagiliaji waliopewa mashamba kuyakodisha kwa watu wengine.

"Mhe. Mkuu wa Mkoa sisi huu udongo unatuchanganya sana tunashindwa kuelewa tulime mbegu gani tunaomba mtusaidie kutupimia udongo wetu" Alisema Chacha.

Aliongeza kuwa baadhi ya wasimamizi wa skimu hiyo sio waaminifu kwa wanachama wao jambo linalopelekea washindwe kufanya shughuli za kilimo cha umwagiliaji akisema kuwa baadhi wamekuwa wakikodisha mashamba na kuwanyima fursa wengine.

Akisoma taarifa ya mradi huo Mwenyekiti wa Umoja wa umwagiliaji Itagata Stephen Mbonge alisema kuwa mashamba yenye ukubwa wa Ekari 209 yaligawiwa kwa wanachama 321 ekari 106 ziligawiwa kipindi cha masika mbunga ekari 73 na kutoa tani 105.7 na mazao mengine ekari 33 ambazo zimetoa tani 28.19 lakini kipindi hiki cha kiangazi ekari 40 tu ndizo zimelimwa zikiwa na mazao mchanganyiko na hazijavunwa.

Baada kusomewa taarifa ya mradi wa Skimu ya Umwagiliaji Mkuu wa Mkoa Serukamba akafika  kuzungumza na wananchi wa kijiji cha Itagata msisitizo wake ukiwa katika kuendeleza mashamba yaliyopo kwenye skimu hiyo, kushiriki kwenye zoezi la Sensa Agosti 23 mwaka huu na kuwataka wananchi wa kijiji chicho kukata Bima ya afya ambayo imekuwa ndio wimbo wake tangu aanze majukumu yake Mkoani Singida.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.