• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

RC Serukamba awahubiria Madiwani Mkoani Singida uadilifu na ushirikiano.

Posted on: September 6th, 2022

Madiwani wa Halmashauri za Wilaya zote za Mkoa wa Singida wametakiwa kufanya kazi kwa uadilifu na kushirikiana hasa katika miradi ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa maeneo mbalimbali Mkoani hapo ili kuimarisha usimamizi wa watendaji katika Halmashauri zao.

Akiongea katika mabaraza mbalimbali ya Madiwani aliyohudhuria leo Mkoani hapo yakiwemo Manispaa ya Singida, Singida Vijijini, na Mkalama kama sehemu ya kujitambulisha, Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba ameonya tabia ya baadhi ya Madiwani kuwa wakusanya kodi na watoa misamaha ya ushuru katika mageti mbalimbali ya kukagua mazao na kuwataka kusimamia majukumu yao ya msingi ya kuwasimamia watendaji.

Serukamba amesema vitendo ambavyo sio vya kiadilifu vikifanywa na viongozi kama Madiwani vitasabisha kiongozi huyo kushindwa kuwasimamia watendaji wa kazi hata kama watakuwa na makosa katika kazi zao.

"Ukimuomba Mhandisi akupe mifuko miwili ya saruji yeye atachukua mitano na hutaweza kumuuliza, ukikusanya kodi wewe watendaji hawataweza kukuuliza na Diwani hutaweza kumsimamia mwingine ambaye alikusanya kodi pasipo kupeleka benki”. Alisema Serukamba

Akiongelea kuhusu msimu wa kilimo RC Serukamba  ameelekeza kwamba  Madiwani wahakikishe kwamba wakulima wanaongeza eneo la kilimo ikilinganishwa na mwaka jana kwa kuwa Serikali imeendelea kutoa ruzuku za pembejeo za kilimo ikiwemo mbegu na mbolea.

Aidha Serukamba amewataka wakulima mkoani hapo kuanza maandalizi ya mashamba mapema ili mvua za kwanza zitumike kwa kupandia kwa kuwa uzoefu wa msimu uliopita ulionesha kwamba waliowahi kupanda walipata mazao ikilinganishwa na waliochelewa kupanda.

Hata hivyo RC amesema kwamba Serikali inatumia kiasi kikubwa cha fedha kuagiza mafuta ya kupikia kutoka nchi za nje ambapo ameeleza kwamba Mkoa wa Singida una uwezo mkubwa kuondoa pengo hilo kwa kuongeza eneo la uzalishaji na matumizi ya mbegu bora za kilimo.

Mkuu wa MKoa wa Singida Peter Serukamba akizungumza na Madiwani pamoja na Watendaja wa Halmashauri ya Wilaya Mkalama 

Akiwa Mkalama Mkuu wa Mkoa amewataka viongozi wa eneo hilo kuhakikisha kunajengwa soko la vitunguu ili kuondokana na changamoto ya walanguzi kuwafuata wakulima mashambani.

Aidha amesema kwa kuwaacha walanguzi kuingia mashambani kumesababisha wakulima kutopata faida inayotokana na kazi yao kwa sababu ya ulanguzi unaofanywa huko shambani.

Hata hivyo Serukba ameendeleza kampeni yake ya kuhakisha kila kaya inakuwa na BIMA ya Afya ya CHF iliyoboreshwa ambapo amewataka Madiwani kusaidia zoezi hilo kwamba hata mwananchi ambaye hatakuwa na uwezo kulipa 30,000 watatoa mifugo kwa ajili ya kupata bima hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskasi Muragili akizungumza wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani.

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Sophia Kizigo akizungumza wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida Yagi Kiaratu akizungumza wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Singida Vijijini Elia Digha akizungumza wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani.

Sehemu ya Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Singida Vijijini

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.