• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

SERIKALI IMETOA BURE MBEGU NA VIUATILIFU KWA AJILI YA KILIMO CHA PAMBA KWA MKOA WA SINGIDA.

Posted on: November 7th, 2017

  Serikali imeahidi kutoa bure pembejeo za kilimo kwa wakulima mbali mbali wa zao la pambamkoani Singida kuanzia msimu huu wa kilimo ikiwa ni moja ya juhudi za kuhamasishana kufufua kilimo hicho mkoani hapa.  

MkurugenziMkuu wa Mamlaka ya Bodi ya Pamba nchini, Marco Mtunga ameeleza hayo juzi katikavijiji vya Kinyangiri na Lyelembo wilayani Mkalama katika siku ya kwanza yaziara yake ya siku mbili kuhimiza Kilimo cha pamba mkoani Singida. 

Kwamujibu wa Mkurugenzi huyo, Kampuni ya Biosustain iliyopo mjini hapa imepewajukumu la kuleta na kusambaza mbegu na madawa yote yahusuyo kilimo cha pambabure na kwamba gharama ya pembejeo hizo italipwa na Serikali. 

Kutokanana hilo, Mkurugenzi huyo amewataka Wakulima kutumia vyema fursa hiyo kwa kulimamashamba makubwa zaidi lakini pia kwa kuzingatia tija na ubora wa pamba. 

Amesemakuwa Wakulima wataweza kufanya hivyo tu iwapo pia watawatumia kikamilifuwataalamu wao wa kilimo na kufuata Kanuni na Taratibu za kilimo bora. 

“Mmepewaupendeleo maalum, kazi yenu sasa ni kulima tu, malipo ya mbegu na viuatilifuvyote italipwa na Serikali. Hapa hakuna kisingizio cha kushindwa kulima”, amesemaMtunga na kuongeza;

“Pandenivizuri ili wakati mnatumia dawa, kiwango kikubwa cha dawa kisipotee bure maanakama hukupanda kwa mstari lazima kutakuwa na ugumu wa kupulizia mimea yako.Jengeni utamaduni wa kuwatumia wataalamu wa kilimo kama ilivyo kwa wafugajimifugo yao inapopatwa na maradhi”.  

Aidha,amewataka wakulima wa zao hilo kuhakikisha wanang'oa masalia yote ya misitu yapamba na kuichoma moto kwa kuwa, kwa kuacha kufanya hivyo wanaruhusu waduduwaliomo kwenye masalia kuendelea kunenepeana na hivyo kuhatarisha mazao mapyayanayopandwa.  

Mkurugenzihuyo amewasihi wakulima kuacha kuchanganya kilimo cha pamba na mazao mengineakisema kuwa tafiti zinaonesha pamba iliyochanganywa na mazao mengine hutoavitumba vitatu tu ikilinganishwa na vitumba 10 kwa kilimo cha pamba iliyolimwapeke yake. 

Wakulimawa zao hilo wamemueleza Mkurugenzi huyo kuwa, moja ya sababu za kushuka kwauzalishaji pamba kwenye maeneo yao ni pamoja na bei kuwa ndogo kwa kisingiziocha Soko la Kimatafa kushuka na kuchezewa mizani wanazotumia kupima mazao yao,hali inayowapunja kimapato.  

Hatahivyo, wamejibiwa kuwa suluhisho la kuchezewa mizani lipo mikononi mwao ilimradi tu wajenge tabia ya kuhoji mara moja wanapoona mambo yanaenda isivyobadala ya kusubiri hadi siku ya vikao. 

Wakatihuohuo Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amewataka watendaji wote waserikali na Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoani Singida kulima ekari moja ya pambakila mmoja ili kuamsha hamasa kwa wananchi wengine.

DktNchimbi ameongeza kwa kuwataka watendaji hao kuliweka zao la pamba kama ajengakatika vikao vyao, huku akiwataka viongozi wa dini na vikundi vya kwayakuonyesha mfano kwa kulima vizuri pamba.

Ameongezakuwa vijana wanaocheza vijiweni ‘pooltable’ waache mara moja na kujikita katikakilimo cha pamba kwa kuwa ni chanzo kikubwa na cha uhakika cha kujipatia fedhana hivyo kuchangia kukuza uchumi. 

Aidhaamewataka wakulima wa pamba kuwasikiliza wataalamu na sio kupanda kwa mazoeahuku akishauri kuwa mikutano yote inayohusu kilimo cha pamba ifanyike katikamashamba ya wakulima.

DktNchimbi ameeleza kuwa kauli mbiu mpya ya kilimo cha pamba kwa Mkoa wa Singidani, ‘Singida Mpya, kwa Pamba yenye Tija’. 

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.