• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

Serikali Imeupatia Mkoa wa Singida Sh.Bilioni 5.8 Kujenga Vyumba vya Madarasa 290

Posted on: November 1st, 2022

SERIKALI imeupatia Mkoa wa Singida Sh.Bilioni 5.8 ambazo zitatumika kujenga vyumba vya madarasa 290 kwa ajili ya wanafunzi watakaojiunga na kidato cha kwanza kuanzia Januari 2023.

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, alisema hayo hivi karibuni wakati wa kuwekwa Wakfu Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kati, Askofu Dk. Syprian Hilinti.

Kufuatia hali hiyo, aliwagiza wazazi na walezi kuhakikisha wanafanya maandalizi ya kuwapeleka watoto wao shule watakaoanza darasa la kwanza na wale wa kidato cha kwanza kwani Serikali imeweka mazingira mazuri ya kumuwezesha kila mtoto anapata elimu.

Serukamba ambaye alimwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan katika hafla hiyo, alisena Serikali inatambua na kuthamini mchango wa Kanisa la KKKT katika huduma ya Kiroho na kuhubiri Injili ya amani, umoja, upendo na katika kulea na kukuza vipawa mbalimbali.

"Kanisa la KKKT Dayosisi ya Kati pia linatoa huduma mbalimbali za kijamii kama elimu na afya kwa kushirikiana na Serikali, mfano mmojawapo ni hospitali ya Iambi iliyopo Wilaya ya Mkalama ambayo inamilikiwa na Kanisa hilo ambapo Serikali inalipa mishahara ya watumishi  31 ili kuyawezesha malengo ya Kanisa katika utoaji huduma kwa wananchi," alisema.

Kuhusu kufunguliwa njia ya reli ya kutoka Manyoni kuja Singida, alisena Serikali ya mkoa ilishawasilisha ombi hilo kwa Shirika la Reli Tanzania (TRC) kwa ajili ya kufufua njia hiyo na shirika limeahidi kushughulikia.

Alisema katika suala la ujenzi wa uwanja wa ndege wa kisasa upo katika mpango wa Serikali ambapo mkoa ulipokea maelekezo ya kubainisha eneo ambapo uwanja utajengwa.

Alisema changamoto iliyopo ni kwamba eneo la uwanja wa ndege wa sasa limevamiwa na kujengwa nyumba za makazi jambo ambalo linaunyima sifa uwanja huo kutengenezwa kwa hadhi na kiwango cha kisasa.

"Eneo la pili lililobainishwa na kutengwa Kijiji cha Manga linahitaji malipo makubwa ya fidia ili wananchi waliomo ndani ya eneo hilo wapishe kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa ndege," alisema.

Hata hivyo, alisema suala hilo bado Serikali inaendelea nalo na ana imani jawabu litapatikana kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa uwanja wa ndege wa kisasa hasa kwa kuzingatia jiografia ya Mkoa wa Singida ambao ni jirani ya makao makuu ya nchi.

Kuhusu ujenzi wa barabara ya Singida – Hydom – Mbulu alisema  ipo kwenye mpango na utekelezaji wake umeanza ambapo kipande cha Singida – Ilongero – Hydom chenye urefu wa KM 93.3 kazi ya upembuzi yakinifu na maandalizi ya kutangaza zabuni zinaendelea.

Aidha, aliwagiza wakuu wa Wilaya za Singida na Iramba kushughulikia migogoro ya ardhi maeneo ya Kititimo, Ruruma na Ushora na kumpa taarifa ifikapo Novemba 30, mwaka huu ambao Kanisa la KKKT lililalamika kuwa maeneo hayo ambayo ni mali ya Kanisa yamevamiwa.

MWISHO

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.