• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

SERIKALI KUWAUNGANISHA WAZALISHAJI WAKUBWA WA CHAKULA KATIKA KATA TANO WILAYANI IRAMBA..

Posted on: July 2nd, 2017

  Serikali imedhamiria kuwaunganisha wakulima wakubwa wa mazao ya chakula wa kata tano za Wilaya ya Iramba kwa kujenga daraja na makaravati manne katika barabara yenye urefu wa kilomita 38.6 yatakayo gharimu shilingi bilioni 4.1.

Akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa daraja la Mto Mtoa na makaravati katika barabara ya shelui-Mtoa-Urughu Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Amour Hamad Amour amesema serikali imedhamiria kuwaunganisha wananchi ili wazalishe mazao, waanzishe viwanda kisha kusafirisha bidhaa.

Amour amesema kwakuwa barabara hiyo inahudumia wananchi wa  kata za Shelui, Mtoa, Mtekente, Urughu na Ndago wananchi wa maeneo hayo watumie fursa ya kuwa na barabara nzuri kwa kutengeneza viwanda vidogo, vya kati na vikubwa na kisha kusafirisha bidhaa na sio mazao kama mali ghafi.

Amesema kwa kufanya hivyo wakulima wa mazao wataweza kujiongeza kipato chao kwa kuwa hawatapunjwa kwa kuuzwa mali ghafi ambayo hupelekwa kwenye viwanda vya nchi nyingine hivyo barabara hiyo iwe hamasa kwao kuzalisha kwa wingi pamoja na kuanzisha viwanda  kwa wingi.

Mradi huo wa barabara na makaravati unatekelezwa kupitia mpango wa kuondoa vikwazo kwenye barabara za vijijini, mpango unaofadhiliwa na serikali ya Tanzania kwa kushirkiana na serikali za Uingereza na Ireland Kaskazini.

Kukamilika kwa ujenzi wa daraja na makaravati hayo kutawezesha barabara hiyo kupitika kwa kipindi cha mwaka mzima na hivyo kuwanufaisha wakazi elfu 79 wa kata hizo pamoja na kuwezesha utoaji wa huduma za kijamii katika eneo hilo lenye shule za msingi 29, shule za sekondari 6, zahanati 7 na kituo cha afya kimoja.

Wakati huo huo Kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru Amour Hamad Amour amezindua mradi wa ghala la kuhifadhia chakula katika kijiji cha Nselembwe ambalo litakuwa likihudumia jamii ya kata za Ulemo,Mgongo, Ntwike, Shelui na Mtoa.

Akifungua ghala hilo Amour amesema kauli mbiu ya mwenge wa uhuru mwaka huu ni shiriki kukuza uchumi wa viwanda kwa maendeleo ya taifa hivyo ujenzi wa ghala ili kuhifadhi mazao unasaidia wananchi kutoyauza ovyo mazao na kuyahifadhi mahali salama kabla ya kuyachakata kuwa bidhaa.

Amesema mradi huo wenye thamani ya shilingi milioni 350 utaweza kuwasaidia wananchi kuhifadhi mazao kwa mfumo wa stakabadhi ghalani na kuwa na kauli moja juu ya bei ya mazao pia watakua na uhakika wa mazao.

Amour amewasisitiza wananchi wa kata hizo kuzalisha kwa wingi kwa kuwa sasa wana uhakika wa sehemu salama ya kutunzia mazao yao ili wasishawishike kuyauza kwa bei ndogo.

Mwenge wa Uhuru ukiwa Wilayani Iramba umetembelea miradi yenye thamani ya shilingi bilioni 4.8 huku ukipitia miradi 6 na kuona shughuli 5 katika vijiji  10 na tarafa 4 katika umbali wa km 119.1.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.