• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

Serukamba amaliza mgogoro wa shamba Yulansoni uliodumu kwa zaidi ya miaka kumi.

Posted on: January 23rd, 2023

Uongozi wa Kijiji cha Yulansoni katika Kata ya Kinyangiri Wilayani Mkalama Mkoani Singida wameagizwa kuwarejeshea  wakulima mashamba wanayogombania  kwa kuwa hawana vielelezo vya kutosha vinavyoonesha kuwa  waliwakodishia wananchi hao mashamba hayo kwa mikataba.

Agizo hilo limetolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi hiyo baada ya kukutana na viongozi na wazee wa Kijiji hicho pamoja na uongozi wa Wilaya ya Mkalama.

Amesema yupo mwananchi ambaye ni mjane anayelalamikia kuzuiliwa kutumia ardhi yake ambayo alifyeka wakati likiwa shamba pori toka mwaka 1988 lenye jumla ya ekari 65 ambapo viongozi wa kijiji hicho walidai kwamba walimkodishia kwa mkataba wa miaka nane (8) jambo ambalo RC Serukamba alitaka Ofisi ya Kijiji kuwasilisha muhutasari wa vikao  na mkataba wa makubaliano hayo.

Aidha, Kijiji kiliwasilisha bàadhi ya nyaraka ambazo baadhi zinaonesha maandishi ambayo yanamtaja mjane huyo badala ya mume wake ambaye ndio alikuwa mmiliki wa shamba hilo, ambapo  RC Serukamba alisoma nyaraka hizo na kuonekana ziliandikwa mwaka 2005 badala ya 1998 ambapo marehemu ndipo alipofyeka shamba hilo.

Hata hivyo upande wa mlalamikaji uliendelea kudai kwamba Kijiji hicho kinahitaji shamba hilo ambalo sio mali yake ili kulikodisha ambapo tayari walishachukua fedha ambapo wanatakiwa akimkabidhi shamba au kurudishiwa fedha zake.

Kwa upande wake OCD wa Mkalama alikiri kwamba walipata malalamiko ya mwananchi huyo dhidi ya Kijiji cha Yulansoni ambapo walibaini mwananchi huyo aliachiwa shamba hilo na marehemu mume wake ambaye naye alipata kwa kufyeka pori huku Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Asia Mesos akieleza kwamba aliwakutanisha mdai na mdaiwa ambapo maelezo ya wote wawili yanabainisha kwamba mwananchi huyo anamiliki eneo hilo.

Kutokana na maelezo hayo RC Serukamba aliwataka viongozi hao kuliachia shamba hilo kwa mwananchi huyo aweze kuendeleza shughuli zake za kilimo na kama hawajaridhishwa na uamuzi huo waende Mahakamani.

Naye Miwani wa Kata ya Kinyangiri Emanuel Kabea alimuomba RC kutembelea eneo lingine ambalo na lenyewe lina migogoro na Kijiji ambapo mwananchi aliyefahamika kwa jina la Edward Mnoma alichukua shamba hilo lenye ukubwa wa ekeri Mia moja (100) ambalo lilikuwa ni eneo la hifadhi ya Msitu wa Kijiji na akaliuza ambapo kwa sasa limebaki ekari 30 tu.

Aidha Diwani huyo amemuomba RC kutembelea eneo hilo na kuona kama ekari hizo 30 zilizopo  zinaweza kubaki katika umiliki wa Kijiji hicho jambo ambalo RC Serukamba aliahidi kutembelea eneo hilo baada ya wiki ijayo kupita.

Wakimalizia mjadala huo viongozi hao wa kijiji walimueleza Mkuu wa Mkoa huyo kwamba watarejesha shamba hilo kwa mlalamikaji huku wakijipanga ili kwenda kutafuta haki yao Mahakamani.

Mjadala huo ni muendelezo wa zoezi la utatuzi wa kero za Wananchi zilizotokana na ziara zake katika Halmashauri zote za Mkoa huo ambapo aliwasikiliza wananchi kwa kipindi cha Siku nne mfululizo.

Mwisho

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.