• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

SINGIDA KUKABILIANA NA TATIZO LA MAFUTA YA KULA NCHINI

Posted on: August 8th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba, amesema kuwa Singida imejikita katika kilimo cha alizeti ili kuhakikisha inazalisha kwa wingi mafuta ya kula yanayotokana na zao la alizeti kwa lengo la kupunguza uagizaji wa mafuta ya kula kutoka nje ya nchi.

Mkuu huyo ametoa maelezo hayo leo (tarehe 8 Agosti, 2023) wakati wa kilele cha maadhimisho ya maonesho ya Wakulima, Wafugaji na Uvuvi yaliyohitimishwa Kanda ya Kati katika viwanja vya Nzuguni Jinini Dodoma.

Amesema kuwa Mkoa wa Singida umejipanga katika kilimo cha mazao ya kimkakati ikiwemo kilimo cha zao hilo lengo kubwa likiwa ni kuhakikisha Mkoa huo unakuwa na mafuta ya kutosha kwa soko la ndani na nje hatua hiyo itakuwa imepunguza kwa kiasi kikubwa gharama ya uagizaji wa mafuta hayo kutoka nje ya nchi.

“Mkoa wa Singida unategemea kilimo kwa asilimia 80 na wakazi wake wamekuwa wakijikita zaidi katika kilimo na kwa maana hiyo tunahitaji kuwa na kilimo cha kimkakati ambacho kitaweza kuwainuwa wakulima kiuchumi kwa kuwaongezea kipato wao wenyewe na taifa kwa ujumla” ameeleza Mkuu huyo wa Mkoa.

Aidha amesema kuwa Singida na Dodoma wamejipanga kufanya kilimo chenye tija ambacho kitaifanya mikoa ya Singida na Dodoma kuwa kitovu cha chakula nchini kwa kutumia kilimo cha umwagiliaji katika skimu ya umwagiliaji zilizopo jambo ambalo litanyanyua uchumi wa Mkulima mmoja moja na taifa kwa ujumla wake.

Hata hivyo Serukamba amempongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassani kwa kuwekeza nguvu nyingi kwenye kilimo kwa maana ya kutoa pesa nyingi ambazo zitasaidia ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji pamoja na kuwekeza katika uboreshaji wa pembejeo za kilimo, mifugo kwa njia ya uboreshaji wa majosho.

Amesema kitendo cha Rais Dk. Samia kuwekeza katika kilimo kitasaidia kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazosababishwa na mabadiliko ya tabia ya nchi kwa kusababisha kuwepo kwa mtawanyiko wa mvua ambazo hazieleweki.

“Kutokana na juhudi kubwa za Rais wa awamu ya sita kwa kuona umuhimu wa kuwekeza pesa nyingi kwenye kilimo, Serikali ya Singida kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imejipanga kuhakikisha inalima kilimo chenye tija na siyo kilimo cha kujikimu”

“Hata hivyo niwashauri Mabalozi kuhakikisha wanahamasisha kwa kuwatafuta wawekezaji wakubwa kuja nchini na kujenga viwanda vikubwa vya alizeti kwa ajili ya kuongeza mnyororo wa thamani na kwa kufanya hivyo vitajengwa viwanda vingi vya kuzalisha mafuta hayo na kusababisha uwepo wa mafuta ya kutosha”amesema Serukamba.

Sambamba na hayo amewapongeza washiriki wa makongamano ya maadhimisho ya kilimo, ufugaji na uvuvi kwa kushiriki semina na mafunzo mbalimbali ya kilimo cha Alizeti, Mtama na ufugaji wa Kuku pamoja na kutembelea mabanda mbalimbali kwa ajili ya kujifunza kilimo chenye tija na chenye kuwaletea manufaa.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.