• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

SINGIDA YAADHIMISHA SIKU YA WAZEE DUNIANI, WAZEE 100 WAPATIWA BIMA YA AFYA

Posted on: October 1st, 2023

Mkoa wa Singida leo tarehe 1 Oktoba, 2023 umeadhimisha Siku ya Wazee Duniani kwa kuwapatia Bima ya Afya ya Jamii iliyoboreshwa (iCHF) Wazee miamoja (100) wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo na kuhusisha wawakilishi kutoka Halmashauri zote saba za Mkoa huo.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Singida katika Siku ya Wazee Duniani Jimson Mhagama ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni amesema suala la Wazee kupatiwa vitambulisho vya matibabu ni agizo la Serikali ili kuhakikisha wanatambuliwa na kupewa  huduma stahiki.

Aidha, Mhagama amepongeza hatua nzuri iliyofikiwa katika uundwaji wa mabaraza ya wazee ambapo mabaraza ya Wazee 637 kati ya hayo mabaraza 151 sawa na asilimia 24 yamejengewa uwezo katika Mkoa wa Singida ili kuhakikisha huduma na maslai ya Wazee yanapatikana.

“Niwapongeze sana wadau wetu wa maendeleo kwa kazi kubwa mliofanya ya kuhakikisha wazee wanajengewa uwezo wa Sera ya wazee ya mwaka 2003 pamoja na majukumu ya viongozi wa mabaraza ya Wazee katika ngazi mbalimbali”

“Nawaelekeza Wakurugenzi wote wa Halmashauri kuhakikisha mabaraza ya Wazee yanafanya vikao vyao kila robo kama miongozo inavyoelekeza ili kuwezesha ufanisi katika kazi zake”. Amesema Mhagama kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba.

Serukamba ametoa rai kwa Jamii hasa ndugu wa karibu kuacha tabia ya kuwanyang’anya Wazee maeneo yao (ardhi, nyumba nk) jambo linalopelekea Wazee kukosa mwelekeo. Hivyo amesisitiza kuwa kitendo hicho ni kinyume na Sheria, na wale watakaobainiki Sheria itachukua mkondo wake.

Akizungumzia suala la malezi ya watoto, Mhagama kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo amesisitiza umuhimu wa wazazi kuwalea watoto wao ili kuwajengea stadi mbalimbali za maisha na kufanya wawe raia bora.

Kwa upande wa wazee wanaonufaika na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF Serikali Mkoani Singida imesajili kaya zipatazo elfu 58,760 zinazonufaika wakiwemo wazee, kati ya kaya hizo watoto ni elfu 1,318 kutoka kaya maskini ni wanufaika wa mfuko huo.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba kupitia kwa mwakilishi wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni ametoa wito kwa vijana kuwatunza wazee wao ambao ni hazina kwa kuwatimizia mahitaji yao mbalimbali ikiwemo chakula ili kuepuka Wazee kuzunguka mitaani wakiombaomba.

Akimalizia hotuba yake Mkuu wa Mkoa wa Singida iliyosomwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni amewakumbusha na kuwaomba wazee kuendelea kusisitiza suala la malezi chanya kwa watoto na maadili mema kwa vijana ili kujenga jamii isiyokuwa na mmomonyoka wa maadili.

Mkoa wa Singida unandelea kuboresha huduma za Afya kwa Wazee, huduma za matunzo kwa Wazee wasio kuwa na uwezo kwa kuwatengea makazi yaliyopo Sukamahela katika Wilaya ya Manyoni Mkoani humo.

Kauli mbiu ya mwaka huu (2023) ambayo ni “Uthabiti wa Wazee kwenye dunia yenye Mabadiliko.

“Kauli mbiu hiyo inamaanisha kuwa Dunia inapitia mabadiliko mbalimbali ya kiuchumi, kijamii, kiutamaduni, kisiasa na dhihiri kuwa Wazee wamekuwa imara kwenye kukabiliana na mabadiliko hayo”.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.