• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

TEMESA waagizwa kujitangaza ili kuongeza wateja

Posted on: March 29th, 2023

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Fatma Mganga ameiagiza Taasisi ya Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) kujitangaza kwa kufanya kazi zenye ubora na kutafuta wateja wapya badala ya kutegemea Serikali na Taasisi zake.

Kauli hiyo ameitoa leo tarehe 29.03.2023  wakati wa ufunguzi wa kikao cha wadau wa TEMESA kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hizo zilizopo Singida mjini ambapo amesema Serikali imetoa mashine na mitambo mbalimbali kwa taasisi hiyo  ambazo zinaweza kuwa sababu ya kimbilio kwa wateja wa nje endapo huduma itaboreshwa kwa kiwango kikubwa.

Dkt. Mganga ameagiza taasisi hiyo kufanya utafiti na kubaini sababu zinazosababisha upatikanaji hafifu wa wateja huku akibainisha kwamba uboreshaji wa huduma kwa mteja utasaidia kwa kiasi kikubwa Taasisi hiyo kufanya kazi ki biashara.

"Kwa vifaa ambazo Serikali imevileta tunategemea TEMESA iwe kimbilio kwa watu wengi, tangazeni kazi zenu muongeze wateja wa nje ya Serikali na hakikisheni mnaboresha huduma kwa wateja wavutiwe" Dkt. Mganga

Aidha amewataka kuacha kufanya kazi kwa mazoea ili kuondoa malalamiko ambayo yalikuwepo awali yaliyohusu upatikanaji wa vipuri, matengenezo kuchukua muda mrefu na gharama kubwa ya matengenezo ambapo amewataka kuhakikisha wanakabiliana na hali hiyo na kununua vitu kwa pamoja (balk procurement) ili kupunguza gharama kwa wateja.

"TEMESA imeanzishwa ili kutoa unafuu wa utenegenezaji wa magari na umeme pamoja na mitambo kwa bei nafuu kuliko wengine hivyo niwapongeze kama mmeanza hatua za mabadiliko"

Hata hivyo RAS ameishauri Taasisi hiyo kupitia kitengo chake cha usimikaji wa umeme kuandaa mkakati wa kupima umeme katika majengo ya Serikali na  Taasisi mbalimbali na kutoa ushauri kwa wamiliki ili kuondoa changamoto za ajali za moto ambazo mara nyingi zimekuwa zikielezwa  kuwa zinasababishwa na hitilafu za umeme.

Hata hivyo  Dkt. Mganga amesisitiza watumishi hao kuhakikisha wanakuwa waaminifu katika kutunza na kutumia mali za Umma na kuwekeza katika matumizi ya TEHAMA katika uhifadhi na ugawaji wa vipuri ili kuepusha upotevu.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa TEMESA Mhandisi Hassani Karonda amesema katika kuboresha huduma zao Serikali katika mwaka wa fedha kwa mwaka uliopita ilitoa milioni 700 kwa ajili ya uboreshaji wa miundombinu lakini ambapo kwa mwaka wa fedha ujao wametenga Bilioni moja kwa ajili ya kuendeleza uboreshaji huo.

Awali akitoa taarifa ya kikao kazi hicho  Erasto Cheza fundi mkuu wa Karakana Mkoa wa Singida amesema majukumu ya karakana yao ni kufanya matengenezo ya magari pikipiki na mitambo ya Serikali, utenegenezaji na usimikaji wa mifumo ya Umeme na viyoyozi na ameendelea kueleza kwamba wanatoa ushauri wa kitaalamu nyanja za Mhandisi wa ufundi na umeme.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.