• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

Tushirikishe viongozi katika utekelezaji wa miradi ya TASAF - RC. Mahenge

Posted on: May 28th, 2022

Ushirikishwaji mdogo wa Viongozi wa Wilaya na Wakurugenzi wa  Halmashauri katika utekelezaji wa miradi ya TASAF  kunasababisha miradi hiyo kutokamilika kwa wakati na kushindwa kufikia malengo yalikusudiwa.

Waratibu wa TASAF katika ngazi za Wilaya hawatoi taarifa kwa viongozi wao na kwa Wakurugenzi wa  Halmashauri badala yake wanatuma taarifa moja kwa moja kwa waratibu wa kitaifa jambo ambalo limekuwa likiongeza changamoto za kiusimamizi.

Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge alipohudhuria mafunzo ya mifumo mbalimbali ya uendeshaji miradi ya TASAF yaliyofanyika katika Hotel ya KBH iliyopo mjini hapo.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge akizungumza na Viongozi wa Sekretarieti ya Mkoa, Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri (hawapo pichani) waliohudhuria mafunzo ya mifumo mbalimbali ya uendeshaji miradi ya TASAF.

RC Mahenge amebainisha kwamba katika miradi hiyo kuna fedha zinazotolewa kwa ajili ya ufuatiliaji lakini viongozi hawawezeshwi jambo ambalo limekuwa likisababisha miradi kutopata usimamizi unao stahili.

“Ipo miradi ya kijamii kama mabwawa au malambo ambapo kulihitaji kuongezewa nguvu kidogo na Halmashauri kwa kuwa baadaye watachukua ushuru na ajira kwa watu hao zingeongezeka na  wangehitimu mapema" alisema RC Mahenge.

Serikali inatoa fedha nyingi  katika miradi ya TASAF ambazo kama wakiachiwa waratibu peke yao kuna uwezekano mkubwa wa malengo kutofikiwa hivyo niwaombe wakuu wa Wilaya  msaidie kusimamia ili wananchi waweze kunufaika.

Akimalizia hotuba yake Mkuu wa Mkoa amewataka waratibu kuendelea kutoa elimu kwa Wananchi kuhusiana na uendeshaji wa Miradi hiyo kwa kuwa jamiii imekuwa na maswali mengi hasa katika ajira za muda na namna ya ulipaji wa fedha zao.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida Yagi Kiaratu ameipongeza Serikali kwa kuongeza idadi za wanufaika katika miradi hiyo huku akibainisha uwepo wa changamoto kadhaa za kimfumo zikiwemo baadhi ya wanufaika kukosa sifa kwa sababu ya kuwa viongozi na kuomba jambo hilo liweze kuangalia vizuri.

Mafunzo yakiendelea

Katika Mafunzo hayo yaliwahusisha wenyeviti wa Halmashauri ambao kwa nyakati tofauti nao walionesha baadhi ya changamoto katika maeneo na kuomba TASAF makao makuu kuangalia namna ya kuzitatua.

Awali akitoa taarifa ya Mradi wa TASAF awamu ya pili Kaimu Meneja wa malipo kwa walengwa na uhaulishaji fedha Kitaifa Msangi Tsetonga amebainisha kwamba  Mradi una gharama ya Dola za Kimarekani 883.31 sawa na Trilioni 2.03 ambayo ni sawa na asilimia 0.5 na walengwa ni Milioni 1.45 ambao utambuzi ulifanyika katika Vijiji zaidi ya 6000.

Bwana Msangi amesema tathmini inaonesha kwamba kuna Kaya zenye uwezo wa kufanya kazi zipatazo 979,918 sawa na asilimia 67 wakati familia zenye uwezo wa kufanya kazi lakini hazina watoto ni 190,988 sawa na asilimia 13.2 ki Taifa. 

Mratibu huyo akabainisha kwamba jumla ya Kaya 179,821 sawa na asilimia 12.4 ni Kaya za wazee walemavu na wagonjwa wa muda mrefu na hazina watoto.

Mafunzo hayo yalihudhuriwa na wakuu wa Wilaya wenyeviti wa Halmashauri Wakurugenzi wakuu wa Idara na waratibu wa Mradi.


MATUKIO KATIKA PICHA

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida Yagi Kiaratu (kushoto) pamoja na Wenyeviti wa Halmashauri za Wilaya wakishiriki Mafunzo hayo.

Sehemu ya Sekretarieti ya Mkoa wa Singida wakishiriki Mafunzo hayo.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.