• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

*WAKUU WA IDARA YA KILIMO KIKAANGONI KWA KUTOWAFIKIA WAKULIMA

Posted on: November 30th, 2024

Wakuu wa Idara za Kilimo Mkoani Singida wamepewa muda wiki mbili kuhakikisha wanaandikisha wakulima katika daftari la kilimo kufikia asilimia 85 au zaidi Kwa lengo la kuhakikisha wakulima wanapata huduma ya mbegu na mbolea za ruzuku kuelekea Msimu mpya wa kilimo.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe.Halima Dendego wakati wa kikao Cha mrejesho wa wadau sekta ya kilimo kutathimini uandikishaji wa wakulima ambapo halmashauri zote za Mkoani Singida ziliwasilisha utekelezaji wa uandikishaji huo umefikia hatua gani ili kurahisisha upatikanaji wa mbegu na mbolea kuelekea Msimu wa kilimo ulionza sasa.

Akizungumza katika kikao hicho,Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe.Halima Dendego amesisitiza utendaji WA kazi Kwa bidii Kwa vitendo zaidi kuliko mikakati ya maneno isiyo ya vitendo akiwataka kutoka mijini na kuwafuata wakulima maeneo Yao mpaka vijijini wanapoishi ili kuwa rahisi kuwapata na kuwapatia elimu ya kilimo wakati wa kuwasajili.

"Msirudi nyuma,rudini kazini mkawe sababu ya wakulima wetu kufanya vizuri kwasababu tunataka kuona kilimo chenye tija kufikia Disemba 31 iwe asilimia mia moja.Tujitume wenyewe na tusisubiri maelekezo kutoka Kwa viongozi wa juu Bali tuende mpaka vijijini walipo tuwafikie Kwa urahisi na tuwape elimu ya kilimo juu ya mbegu na mbolea za ruzuku."amesema RC Dendego

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama,Mhe.Moses Machali akizungumza katika kikao hicho amesema ni wazi kuwa wanalo jukumu kubwa la kuhakikisha wakulima wanajisajili hivyo amewashauri wakurugenzi kuvutumia vizuri vyama vya ushirika na  AMCOS kurahisisha ufikiwaji mzuri na wa uhakika k a mkulima kuhudumiwa huku akisisitiza matumizi ya mfumo WA uandikishaji kiteknolojia katika simu ili kuwafikia wakulima wengi Kwa wakati mfupi.

Naye Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Kilimo na uzalishaji Bw Starnslaus Choaji amemhakikishia Mkuu wa Mkoa kufanyia kazi Yale yote yaliyoazimiwa katika kikao hicho na kuwataka wakuu wa Idara ya kilimo kukutana na kutatua changamoto zote zitakazojitokeza na kuonekana kikwazo katika kufikia malengo yaliyowekwa.

Pia amesema kuwa ni vema kuwahisha mbegu Kwa wakulima kwani mvua zinatarajiwa kuwa chini ya kiwango mwaka huu na kuainisha mawakala mbali mbali ambao wapo tayari kufanya nao kazi Kwa bei rafiki Kwa wakulima kumudu gharama na upatikanaji wa haraka.

Akizungumza baada ya kikao,Bw.Eli Jackson Muna kutoka Wilaya ya Ikungi Kata ya Ntutu amesema wakulima wanategemea mbegu na mbolea za ruzuku kuwahishwa mapema katika maeneo Yao ili kuweza kuzipata na kupanda mapema Kutokana na Hali ya hewa iliyopo huku akiomba mzunguko wa kupata huduma hiyo kuwa mfupi Ili kumfikia mkulima Kwa haraka zaidi.

Katika Mkoa wa Singida mpaka sasa wakulima 108,506 sawa na asilimia 34 wameandikishwa kati ya malengo ya wakulima 316,684 yaliyowekwa huku upatikanaji wa mbegu za alizeti ukiwa Tani 105 kati ya Tani hitajika 1206 na mahindi yakihitajika Tani 316,684.Mbolea mahitaji ni Tani 15,834 huku ikitumika Tani 3,501.





Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.