• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

WANAWAKE WA SINGIDA WAHIMIZWA KUACHA WOGA, WAPIGANIE HAKI ZAO.

Posted on: August 28th, 2017

  Wanawake Mkaoni Singida wamehimizwa kujenga utamaduni wa kujiamini na kuondoa woga, ili waweze kufanikiwa kupigania haki zao za msingi, ikiwemo ya haki ya kumiliki ardhi.

Wito huo umetolewa na diwani wa kata ya Mungumaji Hassan Shabani Mkata, wakati akichangia mada juu ya haki ya umiliki wa ardhi kwa wanawake kwenye mafunzo yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kituo cha walimu mjini hapa.

Mafunzo juu ya haki ya mwanamke kumiliki ardhi yaliandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la Singida IR Vicoba Net Work (SIRVICONET) na kufadhiliwa na shirika la The Foundation for Civil Society kwa ajili ya wanawake wa Singida.

Mkata amefafanua kuwa katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua uhalali wa umiliki ardhi kwa wanawake, isipokua wanawake wenyewe wanakosa haki hiyo kutokana na woga wao uliopitiliza.

Amesema umefika wakati sasa wanawake wawe mstari wa mbele kupingania haki zao na kutokomeza mila kandamizi, ziliyopitwa na wakati ambazo zinawakandamiza kwamba hawana haki ya kumiliki ardhi.

“Kwa hilo wanawake watafanikiwa tu endapo wataondoa woga, wakajiamini na wakaunganisha nguvu zao. Nasisitiza, wanawake wanapaswa kutambua kuwa wanahaki sawa na wanaume, katika kumiliki ardhi”, amefafanua.

Naye mwezeshaji wa mafunzo hayo Afisa Ardhi kutoka Manispaa ya Singida, Lilian Msasi amesema ardhi ni mali ya umma na imekabidhiwa kwa rais, kwa niaba ya Watanzania wote.

“Raia wote…. wanawake na wanaume wana haki sawa ya kupata, kumiliki, kutumia na kugawana ardhi. Miliki za ardhi zilizopo zinatambuliwa na kulindwa kisheria”, amesema Msasi.

Msasi amesema mwanamke ana haki sawa na mwanaume katika kupata, kumiliki, kutumia na kugawa ardhi. Haki hiyo imetamkwa kwenye kifungu cha tatu (92) cha sheria ya ardhi mjini na sheria ya vijiji za mwaka 1999.

Kuhusu sifa za kuomba haki ya kumiliki ardhi, Lilian amesema kuwa ni mtu ye yote mwanamke au mwanaume, mtanzania mwenye umri wa miaka 18 na kuendelea anaweza kupatiwa hati ya kumiliki ardhi.

“Pia kikundi cha watu ambao sio raia wa Tanzania, wanaweza kuomba haki ya kumiliki ardhi (delivative righs), kwa ajili ya uwekezaji”, amesema.

Ameongeza kuwa kwa vile wanawake ni watumiaji wakuu wa ardhi, vyombo vinavyohusika na masuala ya usimamizi na utendaji wa ardhi, vihakikishwe kuwa wanawake na wanaume wanashirikishwa ipasavyo katika masuala yahusuyo ardhi

Awali Mratibu wa Shirika la SIRVICONET, Happy Francis, amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo zaidi wajumbe wa mabaraza ya ardhi ya kata, maafisa watendaji wa kata na maafisa maendeleo ya jamii, ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.

Ameongeza kuwa dhamira ya SIRVICONET ni kuwezesha wanachama wake kuwa na nguvu kiuchumi katika kupambana na umaskini, ujinga na maradhi na kuwa na mahusiano mazuri miongoni mwao.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • "SINGIDA IMEJIPANGA KUONGOZA UFAULU KITAIFA":RC DENDEGO

    June 04, 2025
  • MRADI WA TACTIC KULETA NEEMA MANISPAA YA SINGIDA.

    June 02, 2025
  • "WAHITIMU MSIBWETEKE,JIENDELEZENI KATIKA FANI ILI MJIAJIRI"-DKT.MGANGA

    May 30, 2025
  • DKT.MGANGA:"WATUMISHI MSIKUBALI KUTUMIKA VIBAYA,KUWENI NA UTAMBULISHO MZURI"

    May 27, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.