• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

Wataalam wa Bomba la Mafuta ghafi waanza kazi rasmi mkoani Singida, RC Serukamba awataka kufanya kazi kwa weledi.

Posted on: July 17th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amewataka Wataalam wa kazi ya upimaji wa Mkuza wa Bomba la mafuta ghafi (EACOP) kutoka Kabaale Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani Tanga nchini Tanzania kufanya kwa weledi ili kukamilisha kwa wakati na kupata matokeo chanya.

Serukamba ameyasema hayo leo katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huyo wakati wa ufunguzi wa kikao maalum cha wataalam walioweka kambi mkoani humo kwa ajili ya maandalizi ya kazi ya upimaji wa Mkuza wa bomba hilo lenye urefu wa kilomita 1,443 ikiwa kilomita 2,247 kwa upande wa Tanzania na kilometa 296 kwa upande wa Uganda.

Amesema, Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imedhamiria kuhakikisha miradi yote ya kimkakati inakamilika kwa muda uliopangwa na hili linajidhihirishia kwa wataalam hao ambao wameonekana kuwa na nia na ari itakayowapa msukumo wa kukamilisha kazi hiyo.

“Nina imani mnatambua umuhimu wa mradi huu kwa taifa letu, hivyo katika mikoa linapopita bomba hili na kwa wananchi mmoja mmoja ni toe rai kuwa na moyo wakizalendo tunapoenda kufanya kazi hii ili kuruhusu mradi kutekelezeka pasipo na vikwazo vyovyote hasa vya ardhi” Serukamba

Ameeleza kuwa kwa upande wa Tanzania bomba hilo litapita katika mikoa nane (8) Wilaya 24 na Kata 134 hivyo amesema mradi huo ni wa kipekee katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na unajumuisha ujenzi wa vituo (PS) sita vya kusukuma mafuta ambapo vituo 4 vitakuwa Tanzania na viwili Uganda.

Ameongeza kuwa vituo viwili vya kupunga msukumo (PRS) vitakuwa kwa upande wa Tanzania, Matanki manne yakuhifadhia mafuta yatakayojengwa katika eneo la Chongoleani yenye ujazo wa mapipa laki tano kwa kila moja sambamba na gata la kupakia mafuta ghafi kwenye meli.

Aidha, amefafanua kwamba kutokana na aina ya mafuta (mafuta mazito), bomba litakuwa na mfumo wa upashaji joto kuwezesha mafuta kutiririka kwa urahisi.

Akimalizia hotuba yake Serukamba amesema, bomba hilo ndilo litakalokuwa refu zaidi duniani lenye mfumo wa upashaji joto na huo ndio upekee wake ambapo litajengwa kwa kipindi cha miaka mitatu (3) na uendeshaji wake utachukua takribani miaka ishirini na tano (25) kulingana na kiasi cha mafuta yatakayozalishwa.

Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa amewahakikishia timu ya wataalam hao ulinzi na usalama wa afya zao na vifaa vya utekelezaji wa mradi huo kwa kipindi chote hadi kukamilisha kazi hiyo huku akiwasihi wananchi mkoani humo kutumia fursa la mradi huo katika kujikwamua kiuchumi.

Timu ya Wataalam imeanza kutekeleza rasmi kazi mkoani Singida Julai 14, 2023. imefanikiwa kupima vituo vya kusukuma mafuta, kupunguza kasi ya mafuta na barabara zinazoingia katika vituo hivyo katika mikoa ya Kagera Geita Tabora Singida Manyara na Tanga. Utekelezaji wa upimaji wa njia ya Bomba la mafuta la Afrika Mashariki ni ishara ya kuanza uwekezaji katika uchumi wa nchi na upatikanaji wa ajira.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.