• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

Wawili wauwawa wakidhaniwa ni Majambazi

Posted on: January 24th, 2022

Watu wawili  wanaohisiwa kuwa ni majambazi wamefariki dunia baada ya kupigwa na wananchi wenye hasira kali usiku wa tarehe 23 Januari 2022 Katika Kijiji na Kata ya Ihanja Wilayani Ikungi Mkoani Singida  baada ya kufanya jaribio la kupora Mali ya mfanya Biashara mmoja Katika Kijiji hicho.

Hayo yamesemwa leo tarehe 24 /01/2022 na Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Singida ACP. Stella Mutabihirwa alipokutana na Waandishi wa Habari ofisini kwake  kutoa taarifa ya mauaji hayo ya vijana walioshukiwa kuwa ni majambazi.

Kamanda huyo aliwataja Majambazi hao ni Apolo Issa (32) ambaye ni mkazi wa Puma na Abdi Masoud (45) mkazi wa Mnung’una Katika Manispaa ya Singida ambao walishambuliwa na wananchi wenye hasira kali tarehe 23/01/2022 majira ya saa 3:00 usiku.

Aidha amebainisha kwamba Majambazi hao wamekutwa na Silaha aina ya AK 47 moja na risasi tisa (9) huku wakiwa wanahalimbaya baada ya kupigwa na wananchi wenye hasira kali.

“Watuhumiwa walipofikishwa kituoni, walipekuliwa na mmojawapo aitwaye Apolo Issa katika begi lake alikutwa na Silaha aina ya AK 47 moja ikiwa na risasi tisa (9), huku hali zao zikiwa sio nzuri kutokana na kushambuliwa na wananchi ambapo mtuhumiwa Abdi Masoud alikuwa na jeraha kichwani eneo la kisogoni na mtuhumiwa Apolo Issa akiwa na jeraha kisogoni, usoni na mguuni” Alisema Kamanda wa Polisi

Kutokana na hali hiyo, watuhumiwa walikimbizwa katika hospitali ya Mkoa wa Singida kwa matibabu na walipofika hospitalini Daktari aliwachunguza na kuthibitisha kuwa wamefariki Dunia na ndipo miili yao kuhifadhiwa hospitalini hapo.

Amesema Majambazi hao walikuwa wakifanya jaribio la kupora mali katika duka la mfanyabiashara mmoja ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Ihanja wilayani humo na kwamba watuhumiwa hao walifika katika duka la mlalamikaji majira ya saa 3:00 usiku na kuulizia kama anauza mapanga ambapo aliwajibu hauzi huku mmoja wao akiwa amevalia vazi la Hijabu sura na sauti ikiwa ni ya mwanaume

Akiendelea na taarifa yake Kamanda huyo akabainisha kwamba Mfanyabiaashara huyo aliingiwa na hofu jambo ambalo lilisababisha kupiga simu kituo cha polisi Ihanja na kutoa taarifa kwa viongozi mbalimbali wa Kijiji hicho ambapo wananchi waliamua kuwatafuta na kuwakamata watuhumiwa hao kwa lengo la kuwapeleka Polisi.

Hata hivyo imesemekana baada ya wananchi hao kuwakamata watuhumiwa waliweza kuturoka tena jambo ambalo liliweza kuwakasirisha wananchi hao na kuanza kuwashambulia kwa kutumia silaha mbalimbali za jadi na kuwadhibiti hadi walipofikishwa kituo cha Polisi.

Aidha, Jeshi la Police mkoani Singida limewataka wananchi wa mkoa huo kuacha kujichukulia sheria mkononi pindi wanapobaini uhalifu wa aina yoyote badalayake watoe taarifa kwenye vyombo vya dola ili sheria ichukue mkondo wake.

Hata hivyo Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida linaendelea kuwasihi wananchi kuacha kujitafutia mali kwa njia zisizo halali bali wafanye kazi halali.

Mwisho

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.