• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

WAZIRI MKUU MAJALIWA AHIMIZA MFUMO WA ELIMU YA JUU UANDAE RASILIMALI WATU ILI KUFIKIA TAIFA LA UCHUMI WA KATI.

Posted on: December 1st, 2017

  WaziriMkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassimu Majaliwa Kassim amesemakuna haja ya kuangalia upya mfumo wa elimu ya juu nchini ili kuuboresha uwezekusaidia kutayarisha haraka rasilimali watu walioelimika  zaidi,watakaoliwezesha  taifa kuwa na maendeleo na kufikia uchumi wa kati ifikapomwaka 2025. 

Waziri MkuuMajaliwa ameyasema huyo jana wakati akizungumza kwenye kilele cha mahafali ya33 ya Chuo Kikuu huria cha Tanzania yaliyofanyika kwenye viwanja vya KanisaKatoliki mjini Singida. 

 “Kwakuzingatia malengo ya dira ya taifa ya maendeleo na mwelekeo wa serikali ya awamuya tano, napenda nisisitize kuwa dira ya utendaji wenu ijikite katika maeneoyaliyoainishwa chini ya mwamvuli wa kauli mbiu ya chuo-elimu bora na nafuu kwawote”, amesema. 

Amesisitizakwa kusema kwa uchumi wa kati na wa viwanda, hauwezi kufikiwa au kuwa endelevupasipo kuwa na kiwango cha udahili katika elimu ya juu cha angalau asilimia 23. 

“Hivi sasakiwango cha Tanzania cha udahili katika elimu ya juu ni aslimia nne (4). Kiwangohiki ni kidogo hata kuliko nchi kama Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambaolicha ya hali ya vita nchini mwao kwa muda mrefu,wamefikia asilimia saba (7)”,amefafanua. 

WaziriMkuu Majaliwa amefafanua zaidi kwa kusema kuwa takwimu zinaonyesha kwambakaribu nchi zote washiriki katika jumuiya ya Afrika mashariki, ukiacha Burundi,zina viwango vya juu zaidi vya udahili katika elimu ya juu ikilinganishwa nakiwango cha Tanzania.  

Amesema kwa mujibuwa sera ya elimu ya mwaka 2014 mfumo wa elimu na mafunzo umetawaliwa na muundowa kitaaluma wenye dhana ya kuchuja wahitimu kwa kila ngazi ili kupata wachachewenye uwezo mkubwa katika taaluma. 

“Hali hiiinatokana na nafasi za elimu na mafunzo ngazi za juu kuwa chache kadriwanafunzi wanavyohitimu kuanzia ngazi ya elimu ya msingi na kuendelea. Kwauhaba wa nafasi za elimu ya juu na ufinyu wa bajeti ndio unaosababisha kutumiamuundo wa kuchuja badala ule wa kutoa fursa kulingana na uwezo, vipaji navipawa”, amesema na kuongeza; 

“Huundio mfumo ambao unahitaji kuhuishwa na mfumo wa elimu huria na masafa kamaalivyoeleza Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia Profesa Joyce Ndalichako kwambamazingira, vigezo na masharti ya mchakato huu vimeainishwa katika sera ya elimuna mafunzo 2014’. 

 Wakatihuo huo, Waziri Mkuu Majaliwa amesema serikali inaunga mkono azma ya Wizara yaElimu, Sayansi na Teknolojia ya kuanzisha dawati maalum kwa ajili ya kuimarishamfumo wa elimu huria na masafa.

“Kupitia haflahii, ninaagiza dawati kama hili lianzishwe pia katika Tume ya vyuo vikuu (TCU)na Baraza la elimu ya ufundi (NACTE), kwa lengo la kuhakikisha kuwa taratibuzao za ithibati zinazingatia na kukidhi matakwa ya viwango vya mfumo wa elimuhuria na masafa”, amesema. 

KatikaMahafali hayo Mkuu wa Chuo Kikuu Huria na Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo PeterPinda amemtunuku shahada ya heshima ya uzamivu Balozi Nicolous Kuhanga ambayemchango wake umetajwa kuwa mkubwa hasa wakati wa kuanzishwa kwa chuo hicho. 

Zaidiya wahitimu 2200 wamehitimu katika Chuo Kikuu hicho na kutunikiwa shahadambalimbali ambapo mke wa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Mama Mary Majaliwa, amekuwa miongoni mwawahitimu akitunukiwa shahada ya uzamili katika Elimu ya Utawala, Mipango na Sera.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.