• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC SINGIDA ATOA WITO KWA TANROADS KUWASHIRIKISHA TARURA KWENYE MAFUNZO MAALUM YA KUBORESHA UTENDAJI WA KAZI YANAYOENDELEA NCHI

Posted on: January 30th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi amesema ili kuleta mapinduzi makubwa kwenye sekta ya ujenzi wa miundombinu ya barabara na kukamilisha barabara zote nchini katika kiwango cha lami katika muda mfupi ni muhimu Wakala wa Barabara nchini TANROADS iwashirikishe Wakala wa Barabara vijijini na Mijini (TARURA) kwenye mafunzo maalum ya kuboresha utendaji wa kazi yanayoendelea nchi nzima hivi sasa na kutimiza azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya hapa kazi tu.

Dkt. Nchimbi ametoa rai hiyo leo kwenye ukumbi wa VETA mjini Singida alipohutubia wataalam wa nchi nzima wa Idara ya Manunuzi wa TANROADS walio katika mafunzo maalum ya mfumo rasmi wa kusimamia mahitaji ya raslimali za matengenezo wa barabara (RMMS).

Amesema ameshangazwa kuona katika mafunzo hayo muhimu katika sekta ya uboreshaji miundombinu ya barabara kwa mfumo wa kisasa TARURA hawajashirikishwa wakati mafunzo hayo ni muhimu na yanaongeza tija ya kazi zao.

“Najua nyie mmenolewa vizuri na baba yenu, Rais wetu mpendwa Dkt. John Pombe Magufuli wakati akihudumu katika Wizara yenu, hivyo hakukuwa na sababu yoyote ya kuwaacha wenzenu katika mafunzo hayo ili kubadirishana uzoefu” alisisitiza Dkt. Nchimbi.

Alisema wataalam wa TANROADS wanauzoefu mkubwa ambao kama watabadirishana na kushirikiana na TARURA wataleta mapinduzi makubwa katika sekta hiyo kwani mfumo huo wa RMMS unatumia raslimali chache na kuleta tija kubwa. 


Aidha alisema wakati mwingine kutokana na uzoefu mdogo kumekuwa na changamoto za utengenezaji wa barabara za vijijini kwa wahandisi kuchukua muda mrefu kukamilisha barabara hizo kwa kisingizio cha raslimali fedha ambapo kama wangefundishwa mfumu huu wangeweza kuboresha utendaji wao wa kazi.

Akimkaribisha Mkuu wa Mkoa kuwahutubia wataalam hao, Kaimu Meneja wa TANROADS Mkoa wa Singida, Injinia Matari Masige alisema mafunzo ya mfumo wa RMMS ni nyenzo muhimu kwa tasnia ya ujenzi wa miundo mbinu ya barabara na yanafanyika katika wakati mwafaka.

Alisema kwa mfumo huo wa RMMS hakuna barabara katika nchi ambayo haitafikiwa ambapo pia alisema faida kuu ya mfumo huu unasaidia kutambua mahitaji halisi ya kila barabara hapa nchini.

“Kwa mfumo huu hatutakuwa tena na kitu kama vile hakuna fedha ya ujenzi wa barabara fulani. Sasa tatizo hilo limekwisha” aliongeza Injinia Masige

Mwezeshaji wa mafunzo hayo Injinia Ndaji Mayige alifafanua kwamba kwa mfumo huo kila sehemu korofi zitapata matengenezo kwa wakati na kwamba mfumo huo unarahisisha utoaji wa taarifa za kila eneo.

Alikiri kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa wakala zote mbili na kwamba wataangalia namna bora ya kushirikisha TARURA ili waweze pia kupata mafunzo hayo kwani yatasaidia kuboresha utendaji hadi katika ngazi za vijiji.

Injinia Mayige alisema mafunzo hayo ni ya siku saba ambapo mafunzo kama hayo tayari yameshatolewa kwa kada za Wakuu wa Idara za Mipango na Fedha na Utawala nchi nzima.

Alisema nia ya mafunzo hayo kutolewa nchi nzima ili mikoa yote nchini kuwa na mfumo mmoja utakaorahisisha utendaji.

Matangazo

  • SINGIDA INVESTMENT GUIDE February 23, 2021
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 - MKOA WA SINGIDA December 18, 2020
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2019/2020 SINGIDA RS - GPN 2019 - 2020 August 23, 2019
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2018/2019 September 15, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KATIBU MKUU WIZARA YA AFYA AWATAKA WAZAZI, MAAFISA USTAWI KUWA KARIBU NA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    December 31, 2020
  • TAKWIMU ZAIVUSHA TANZANIA UCHUMI WA KATI- DKT. LUTAMBI

    November 01, 2020
  • UN YAMUUNGA MKONO MAGUFULI KUTOKOMEZA UKATILI WA MWANAMKE IKUNGI

    October 23, 2020
  • VIONGOZI WA DINI SINGIDA WATOA MAAZIMIO MAZITO SABA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

    October 22, 2020
  • Angalia Zote

Video

Baraza la hoja Mkalama 2017
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida. Haki Zote Zimehifadhiwa.