• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

AJALI YA MOTO SOKO KUU SINGIDA YATAFUTIWA UFUMBUZI

Posted on: July 6th, 2025

Serikali ya Mkoa wa Singida imeunda kamati ya kuchunguza na kufanya tathimini tukio la kuungua moto soko kuu la mjini Singida ili wafanyabishara waliopata janga hilo iangalie namna ya kuwasaidia.

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe.Halima Dendego, akizungumza na wananchi na wafanyabishara leo baada ya kutembelea kukagua eneo la tukio, amesema kamati hiyo ifanya kazi hiyo kwa muda wa siku saba kuanzia leo.

Amesema kamati aliyoiunda itawajumuisha wafanyakazi wa serikali, Kamati ya Usalama ya Mkoa na mameneja wa benki zote zilizopo mkoani hapa na kwamba baada ya tathimini hiyo kazi ya kurejesha miundombinu ya soko hilo itaanza mara moja.

“Ndani ya kamati hizi kutakuwa na wataalam wa fedha,wataalamu wa biashara na wataalam wa afya pia kwani wenzetu wamepata mshtuko lazima tuwajue mmoja mmoja wapo wapi ili warejee katika hali salama na kazi hiyo inaanza leo na tumewapa siku saba wamalize kazi hiyo na sisi tutaanza kusafisha eneo hilo kwa ajili ya kujenga kwa haraka,” amesema.

“Naomba nitoe salamu za pole kutoka kwa Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan,  tulimpa taarifa za awali na amenituma tukae mimi na kamati yangu kuweka kambi hapa ili tumjulishe uharibifu uliotokea hapa, lakini pia Waziri wa Tamisemi, Mhe.Mohamed Mchengerwa anawapa pole,” alisema Dendego.

Aidha,Dendego amekipongeza Kiwanda cha Pamba cha Biousastain na kiwanda cha Meru ambavyo vimeweza kusaidia kutoa vitendea kazi katika kufanikisha kazi ya kuzima moto.

Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Martha Mlata, amewapa pole wafanyabiashara kwa janga hilo na kuwaahidi kwamba ana imani kubwa kuwa Serikali itarejesha miundombinu ya soko hilo ili shughuli za biashara ziendelee kama kawaida.

Kadhalika,Mlata amelipongeza Jeshi la Zimamoto na Ukoaji, Jeshi la Polisi na wananchi kwa jinsi walivyoweza kushirikia katika zoezi la uokoaji ambapo hakukuweza kutokea tukio la kupora mali za waathirika.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Singida, Godwin Gondwe, alisema ulinzi utaendelea kuimarishwa katika soko hilo ili uporaji woowote usiweze kufanyika.

Mwenyekiti wa Soko Kuu la Singida, Hassan Mboroo, alisema moto katika soko hilo ulianza kuwaka  saa 3:40 usiku wa kuamkia leo katika duka la kuuza vifaa vya ujenzi baadaye kuenea katika maduka mengine.

Amesema zoezi la kuuzima lilianza kufanyika muda huo na kufanikiwa kuuzima hapo baadae ambapo jumla ya maduka 15 yameteketea kwa moto zikiwamo bidhaa zilizokuwemo na kusababisha hasara kubwa kwa wafanyabiashara.

Mboroo alisema kufuatia tukio hilo kuna haja kwa serikali kuliboresha soko hilo kwa kuweka katika mpangilio mzuri ili kunapotokea majanga kama haya ya moto magari ya kuzimia moto yaweze kupita kwa urahisi kufanya kazi ya uokozi.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • AJALI YA MOTO SOKO KUU SINGIDA YATAFUTIWA UFUMBUZI

    July 06, 2025
  • SINGIDA YATAMBA KWA MAFANIKIO LUKUKI CHINI YA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    July 04, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO KIKAANGONI,WAASWA KUJIPIMA KWA MATOKEO NA SIO IDADI YA VIKAO.

    June 30, 2025
  • HAPO AWALI NA SASA KATIKA MIUNDOMBINU YA ELIMU SINGIDA

    June 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.