• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Miundombinu

SEKSHENI YA MIUNDOMBINU

Seksheni hii ina lengo la kutoa huduma za kitaalamu zinazohitajika kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa katika kuendeleza Miundombinu na inaongozwa na Katibu Tawala Msaidizi ambaye anawajibika kwa Katibu Tawala wa Mkoa.

Majukumu ya Seksheni ya Miundombinu:
•Kuratibu utekelezaji wa Sera, Sheria, Kanuni na Viwango katika nyanja za Barabara, Majengo, Nishati, Upimaji, Ardhi na Mipangomiji
•Kuzijengea uwezo Mamlaka za Serikali za Mitaa katika nyanja za Barabara, Majengo, Nishati, Upimaji, Ardhi na Mipangomiji
•Kuwasiliana/kuwa daraja kuunganisha baina ya Mamlaka zinazohusika kwenye Serikali Kuu na Mamlaka za Serikali za Mitaa juu ya masuala ya Ujenzi
•Kushauri juu ya Masuala ya barabara, Nishati, Ujenzi, Viwanja na uboreshaji mifumo
•Kusimamia na kushauri juu ya kazi za Ujenzi zinazotekelezwa ndani ya Mkoa
•Kuzisaidia Mamlaka za Serikali za Mitaa kutwaa ardhi kwa ajili ya matumizi ya Serikali Kuu
•Kuandaa ramani kwa ajili ya mipangomiji
•Kumshauri Katibu Tawala wa Mkoa juu ya Tathimini ya Athari za Kimazingira
•Kuzishauri Mamlaka za Serikali za Mitaa katika kuendeleza maeneo ya wanyamaporI

Seksheni hii inaongozwa na Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulika na Miundombinu 




UJENZI WA DARAJA LA SIBITI (mita 82) - TANROADS

Daraja la Sibiti liko mpakani mwa Mikoa ya Singida na Simiyu, katika mto Sibiti kwenye barabara ya Mkoa ya Ulemo – Gumanga – Sibiti (km 76). Mradi huu ulihusisha ujenzi wa daraja lenye urefu wa meta 82 na barabara za maingilio ya changarawe (approach roads) zenye urefu wa km 25 kutokea Chemchem hadi Kijiji cha Bukundi Mkoa wa Simiyu. Mradi uligharamiwa na Serikali ya Tanzania kwa asilimia 100. Gharama ya mradi ni Shilingi 28,511,511,000.00. Kazi za ujenzi ilikamilika tangu mwezi  Machi, 2019. Katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali ilitenga jumla ya Shilingi 2,500.000milioni kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara za maingilio ya daraja la mto Sibiti km 25 kwa kiwango cha lami, ikiwa upande wa Bukundi km 5 na upande wa Singida km 20.

 

DARAJA LA MSINGI -TANROADS

kazi ya kumwaga lami nyepezi katika barabara za maingilio ya daraja. Daraja la msingi lina urefu mita 75. Barabara za maingilio zina urefu wa kilomita 1 ambayo ni sawa na mita 500 kila upande wa kuingia darajani. Daraja hili limegharimu shilingi za kitanzania 9,002,573,250.00 kazi  ipo  hatua za mwisho.

Daraja hili linaunganisha barabra itokayo Dar es salaam kwenda Mwanza na Barabara itokayo Iguguno kwenda Nduguti - Gumanga - Ibaga – Bukundi hadi Simiyu.

DARAJA LA MAWE MSINGI - TARURA


Daraja hili lilijengwa mwaka 2018, liligharimu shilingi za kitanzania 250,000,000.00 linaunganisha Tarafa ya Nduguti na Tarafa ya Kinampanda, pia linawezesha njia ya mchepuko kutoka Nduguti kupitia Isinshi na baadae kufika kijiji cha Msingi, barabara hii hutumika pale ambapo mtu anayetoka Kinampanda hataki kufika Gumanga. Mradi huu umetekelezwa na TARURA kwa gharama ya shilingi za kitanzania 222,988,954.00. Daraja lina urefu wa mita 45, upana mita 8 na midomo 4.

DARAJA LA MAWE ENDASIKU - TARURA

Daraja hili ni mradi unaotekelezwa na TARURA. Baada ya matokeo mazuri ya daraja la mawe Msingi TARURA Singida imeongeza ujenzi wa vivuko vya mawe katika Mkoa wa Singida. Kwakuwa Mkoa wa Singida umebarikiwa kuwa na mawe mengi.  Daraja la Endasiku lina urefu mita 30, upana mita 7 na lina midomo 4, limegharimu shilingi za kitanzania 156,601,000.00 linaunganisha kijiji cha Endasiku, Nyahaa, Matala na Mwengeza.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.