• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

*CHANGAMOTO ZA STAKABADHI GHALANI KUTAFUTIWA MAJAWABU,WAKULIMA KUNUFAIKA ZAIDI.

Posted on: November 10th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego, amewatoa hofu wakulima wa dengu katika Halmashauri ya Wilaya ya Itigi kwamba tani 257,933 ambazo bado hazijauzwa kwamba zitauzwa na watalipwa fedha zao.

Akizungumza hayo leo Novemba 10,2024 baada ya kutembelea ghala la kuhifadhia dengu lililopo Itigi mjini, amesema serikali itahakikisha dengu iliyopo inauzwa na kwamba kwa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi hadi sasa zimeuzwa zaidi ya tani 15 000.

"Dengu yetu kutoka Mkoa wa Singida tunauza nchini India,bahati nzuri hadi sasa sijapata malalamiko yeyote ya kwamba labda dengu yetu haina ubora hili jambo la kujivunia,"amesema.

Dendego amesema changamoto ambazo zimepatikana wakati wa utekelezaji wa ununuzi wa dengu kwa kutumia mfumo wa Stakabadhi Ghalani zitaendelea kutatuliwa na kwamba hivi karibuni kutaitishwa kikao cha wadau kujadili namna ya kukabiliana na changamoto hizo.

"Zipo changamoto za ukosefu wa maghala,vyama vya ushirika kufa,mizani na AMCOS  kupitia kikao ambacho wadau ambacho tutakifanya changamoto hizi tutazojadili na kuona namna ya kuzipatia ufumbuzi,"alisema.

Awali Afisa Kilimo Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, Mlagazi Mgalula, amesema zao la dengu limekuwa la kwanza kwa kuingiza mapato kwenye halmashauri ambapo tangu ununuzi ulipoanza Agosti Mosi, 2024 kwa kutumia mfumo wa stakabadhi ghalani wakulima wameweza kulipwa zaidi ya Sh.bilioni 19.

Amesema hivi sasa kuna changamoto ya upatikanaji wa wanunuzi katika dengu iliyopo kwenye ghala na kwamba halmashauri imefanya mipango kutafuta wanunuzi wengine badala ya kutegemea kuuza India tu.

Katibu wa AMCOS ya Mlowa, Emmanuel Daniel, amesema hivi sasa kuna wiki tatu bado minada haijafanyika hali ambayo imezua hofu kwa wakulima hasa ikizingatia kipindi hiki ni cha kuelekea msimu wa kilimo.

Daniel ameiomba serikali kufanya haraka kutafuta wanunuzi katika dengu iliyopo kwenye ghala ili wakulima waweze kulipwa fedha zao na hivyo wapate nguvu kuandaa mashamba yao.

Issa Adam Issa,mkulima anayefaidika na mfumo wa stakabadhi ghalani,ameonyesha kufurahishwa na mfumo huo amesema umekuja kuwanufaisha wakulima na kuhakikisha wanauza mazao yao kwa bei nzuri,ametoa wito kwa serikali kuhakikisha wanaboresha zaidi huduma hiyo ili watu wengi zaidi waweze kujiunga kwa kutumia njia mbalimbali kuwaelimisha hasa kwa kutoa elimu zaidi juu ya mfumo wa stakabadhi ghalani.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.