• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

MIFUMO YA KIDIGITALI KUWAFUNGULIA MILANGO WAJASIRIAMALI

Posted on: December 5th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego, amezindua mafunzo ya kujenga uwezo kwa wajasiriamali kuhusu matumizi ya GS1 Barcodes na QR Codes, akisisitiza kuwa mifumo hiyo ya kidijitali ndiyo njia ya kuwafungulia wajasiriamali milango ya masoko ya kitaifa na kimataifa. Mafunzo hayo yamefanyika chini ya kauli mbiu “GS1 Barcodes: Kiungo chako kwa wauzaji rasmi”, yakilenga kuwajengea wajasiriamali uelewa wa mifumo ya utambulisho wa bidhaa inayotambulika duniani kote.

Semina hiyo imewezeshwa na GS1 Tanzania kwa ushirikiano na taasisi mbalimbali za serikali ikiwemo TRA, BRELA na wadau wengine, ambao wameeleza kwa kina namna wajasiriamali wanaweza kupata barcode na QR code kisheria, hatua zinazowaepusha na ulaghai na kuwalinda dhidi ya matumizi mabaya ya bidhaa zao na makampuni mengine. Aidha, hatua hii ya kidijitali inatarajiwa kuongeza thamani ya bidhaa za Singida na kuziwezesha kupenya kwenye masoko makubwa duniani.

Akizungumza wakati wa ufunguzi, Mhe. Dendego amewataka wajasiriamali wa Singida kuchangamkia fursa hii ya kimkakati, akibainisha kuwa Mkoa wa Singida una bidhaa nyingi zenye ubora wa juu lakini bado hazijapata nafasi ya kutamba kimataifa kutokana na kukosa utambulisho wa kidijitali. “Kundi hili la wajasiriamali ni injini ya uchumi wa Singida. Sisi tuna bidhaa nzuri sana, lakini bila mifumo ya kimataifa kama barcode hatutaifika dunia. Soko la kimataifa linaendeshwa kidijitali, na kama hatuko huko, basi hatutapenya,” amesema.

Ameongeza kuwa Singida ni kitovu cha nchi na hivyo ni mahali sahihi kufunguliwa kwa ofisi ya pili ya GS1 Tanzania. “Ikiwa mtapanga kufungua ofisi mpya nchini, basi Singida ndiyo mahali pake. Tupo katikati ya Tanzania, wajasiriamali watapata huduma kwa urahisi, na hilo litakuwa chachu ya maendeleo makubwa,” amesema.

Mkuu wa Mkoa pia amesisitiza umuhimu wa kulinda amani ili biashara ziendelee kustawi. “Amani ikitoweka, biashara hazipo. Tunaishukuru serikali kwa kutengeneza mazingira bora ya biashara huru. Basi nasi tuitumie fursa hii kutangaza Singida duniani,” amesisitiza.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Rasilimali Watu, Bw. Pancras Stephen, amesema mafunzo hayo yamekuja wakati sahihi, hasa kutokana na ukweli kwamba hata watumishi wa umma wengi wanajihusisha na ujasiriamali. Amesema, “Ujasiriamali wa sasa uko kwenye mifumo ya kidijitali. Tunawaomba mjenge uthubutu na kutumia maarifa haya kupiga hatua katika familia, jamii na taifa.”

Aidha Katibu Tawala Msaidizi – Biashara na Uwekezaji, Bi. Donatira Vedasto, amewataka wajasiriamali kuwa mabalozi wa Singida kupitia bidhaa zao. “Baada ya mafunzo, kila mmoja achukue hatua. Singida inazalisha bidhaa bora sana, lakini bila barcode hatuwezi kufika soko la kimataifa,” amesema.

GS1 Tanzania, kupitia wakufunzi wake, wameahidi kuendelea kutoa mafunzo katika wilaya zote za Singida. Wamesema wajasiriamali wengi wamekuwa wakikosa nafasi ya kuuza kimataifa kwa sababu hawana elimu ya barcode. “Mafunzo haya yatafanya kila mjasiriamali awe na hamu ya kufika soko la kimataifa. Tutafika kila halmashauri kuhakikisha hakuna anayebaki nyuma,”.

Nao Wajasiriamali walioshiriki semina hiyo wametoa shuhuda wakisema matumizi ya barcode yamewasaidia kuaminika katika supermarkets na malls, hatua iliyoimarisha mauzo na kuwapa nafasi ya kutambulika rasmi na serikali. Wameshukuru serikali kwa kuweka miundombinu ya kidijitali na kuwawezesha kufikia masoko makubwa nje ya nchi.

Hatua hii ya kidijitali imeelezwa kuwa mwanzo wa mageuzi makubwa ya biashara Singida, huku serikali na wadau wakiahidi kuendelea kuweka mazingira rafiki kwa ukuaji wa uchumi wa wajasiriamali.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MIFUMO YA KIDIGITALI KUWAFUNGULIA MILANGO WAJASIRIAMALI

    December 05, 2025
  • "WAKURUGENZI HAKIKISHENI MNAFUNGUA OFISI ZA 'TAS' KILA HALMASHAURI"DKT.MGANGA

    November 27, 2025
  • SOKO JIPYA LA VITUNGUU,WAFANYABIASHARA KUPINDUA MEZA KIUCHUMI

    October 20, 2025
  • WANANCHI WAHAKIKISHIWA USALAMA WAO KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

    October 18, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.