• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WANANCHI WAGUSWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA KISHERIA MKOANI SINGIDA

Posted on: January 9th, 2026

Wananchi Mkoani Singida,wamepongeza uzinduzi wa Kliniki ya Huduma za Msaada wa Kisheria uliofanyika Singida, wakisema hatua hiyo itarahisisha upatikanaji wa haki, kupunguza gharama za kufuata huduma za kisheria na kuongeza uelewa wa masuala ya sheria, haki za binadamu na utawala bora kwa jamii.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wananchi walisema kliniki hiyo imewapa fursa ya kupata msaada wa kisheria karibu na walipo, hususan kwa wananchi wa kipato cha chini ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakishindwa kufikia huduma hizo kutokana na umbali na gharama. Walisema huduma hiyo itasaidia kutatua migogoro ya ardhi, ndoa, mirathi na masuala mengine ya kisheria yanayowakabili.

Katika uzinduzi huo, Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe.Dk. Juma Homera, alisema Wizara ina mpango wa kuandaa sera ya kitaifa ya msaada wa kisheria itakayoweka misingi ya kuboresha na kuimarisha utoaji wa huduma hiyo nchini, hatua itakayoongeza upatikanaji wa haki kwa wananchi wengi zaidi.

Dkt. Homera alisema maeneo yatakayoboreshwa ni pamoja na matumizi ya mifumo ya Tehama katika utoaji wa huduma za msaada wa kisheria, kuimarisha utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala na kuweka mifumo madhubuti ya usimamizi ili huduma hizo zipatikane kwa urahisi na kwa wakati.

Alisema utekelezaji wa kampeni ya msaada wa kisheria umeleta mafanikio makubwa, ambapo tangu kuanza kwake wananchi 3,734,157 wamepatiwa elimu kuhusu masuala ya kisheria, haki za binadamu na utawala bora, jambo alilosema linaonesha umuhimu wa kuendelea na huduma hiyo kwa mwendelezo endelevu.

“Huduma ya msaada wa kisheria imekuwa endelevu na itaendelea kutolewa katika halmashauri zote. Serikali itaendelea kuimarisha huduma hizi ili wananchi wajitokeze na changamoto zao zipate ufumbuzi,” alisema Dk. Homera.

Aliongeza kuwa Serikali itaendelea kuanzisha na kuimarisha madawati ya msaada wa kisheria katika ngazi ya halmashauri zote nchini, akibainisha kuwa maafisa wa madawati hayo ni kiungo muhimu kati ya Serikali na wananchi katika kuhakikisha haki inapatikana kwa wakati.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe.Zainab Katimba, alisema halmashauri za wilaya zinapaswa kuweka utaratibu wa kuwawezesha maafisa wa madawati ya msaada wa kisheria ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi, ikiwemo kuwapatia rasilimali na ushirikiano unaohitajika.

Alisema kwa sasa wapo maafisa 446 wa madawati ya msaada wa kisheria katika halmashauri mbalimbali nchini wanaoendelea kutoa huduma hizo, huku akisisitiza kuwa kuimarishwa kwa ushirikiano kati ya halmashauri, wizara na wadau wa huduma za kisheria kutapanua zaidi wigo wa upatikanaji wa haki kwa wananchi.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WANANCHI WAGUSWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA KISHERIA MKOANI SINGIDA

    January 09, 2026
  • MIFUMO YA KIDIGITALI KUWAFUNGULIA MILANGO WAJASIRIAMALI

    December 05, 2025
  • "WAKURUGENZI HAKIKISHENI MNAFUNGUA OFISI ZA 'TAS' KILA HALMASHAURI"DKT.MGANGA

    November 27, 2025
  • SOKO JIPYA LA VITUNGUU,WAFANYABIASHARA KUPINDUA MEZA KIUCHUMI

    October 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.