• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

"WAKURUGENZI HAKIKISHENI MNAFUNGUA OFISI ZA 'TAS' KILA HALMASHAURI"DKT.MGANGA

Posted on: November 27th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Fatuma Mganga, amewaagiza Wakurugenzi wa halmashauri zote mkoani humo wanatakiwa kuhakikisha wanatenga na kuanzisha ofisi za Chama cha Watu Wenye Ualbino (TAS) katika maeneo yao ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa watu wenye ulemavu wa ngozi. 


Dkt. Mganga ametoa maagizo hayo leo Novemba 27, 2025, wakati alipotembelea na kukagua ofisi mpya ya TAS iliyopo katika Manispaa ya Singida, ambapo amesisitiza kuwa uwepo wa ofisi hizo utasaidia kuimarisha uratibu, ulinzi na maendeleo ya kundi hilo.

Amesema kuanzishwa kwa ofisi hizo kunatarajiwa kuleta mageuzi makubwa katika ustawi wa watu wenye ualbino, kwa kuwa zitakuwa kiungo muhimu cha kuwahudumia kupitia ushauri wa kiafya, upatikanaji wa vifaa kinga vya ngozi, miwani maalum na mafunzo ya kujikinga na madhara ya jua.Kadhalika Kupitia huduma hizo, watu wenye ualbino wanatarajiwa kupata nafasi bora ya kujilinda dhidi ya saratani ya ngozi na matatizo ya macho ambayo yamekuwa changamoto kwao kwa muda mrefu.


Aidha, Dkt. Mganga amesema uwepo wa ofisi za TAS katika halmashauri mbalimbali utachangia kupunguza unyanyapaa na ukatili kwa sababu zitakuwa chombo muhimu cha kuendesha kampeni za uhamasishaji na kutoa elimu kwa jamii kuhusu ualbino. Ametaja kuwa ofisi hizo pia zitatoa fursa za kiuchumi kwa watu wenye ualbino kupitia mafunzo ya ujasiriamali, stadi za kazi na kuwaunganisha na miradi ya maendeleo itakayowanufaisha moja kwa moja.


Ameongeza kuwa ofisi hizo zitasaidia kukusanya takwimu sahihi kuhusu mahitaji na changamoto za watu wenye ualbino, hali itakayowezesha serikali na wadau kupanga mipango na kuelekeza rasilimali kwa ufanisi zaidi. Vilevile, ofisi hizo zinatarajiwa kuwa sehemu salama ya kutoa taarifa za vitisho na kupokea msaada wa kisheria au ulinzi wa haraka pale inapohitajika.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TAS Mkoa wa Singida ameishukuru serikali ya mkoa kwa kuwezesha kupatikana kwa ofisi hiyo, akisema itakuwa kitovu cha uratibu na daraja rasmi litakalowaunganisha watu wenye ualbino kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa. Amesema hatua hiyo inatarajiwa kuongeza ushiriki wa kundi hilo katika shughuli za maendeleo pamoja na kuimarisha ushirikiano kati ya serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali na wadau wengine wanaojihusisha na masuala ya watu wenye ualbino.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • "WAKURUGENZI HAKIKISHENI MNAFUNGUA OFISI ZA 'TAS' KILA HALMASHAURI"DKT.MGANGA

    November 27, 2025
  • SOKO JIPYA LA VITUNGUU,WAFANYABIASHARA KUPINDUA MEZA KIUCHUMI

    October 20, 2025
  • WANANCHI WAHAKIKISHIWA USALAMA WAO KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

    October 18, 2025
  • MABINGWA WA CECAFA WAKARIBISHWA NYUMBANI BAADA YA USHINDI MNONO

    October 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.