• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

DKT NCHIMBI ATOA MWEZI MMOJA KWA HALMASHAURI YA IRAMBA KUJENGA VYOO KATIKA MNADA WA MALENDI.

Posted on: October 31st, 2017

  Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amempa mwezi mmoja Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Iramba, kujenga vyoo bora katika Mnada uliopo Kijiji cha Malendi, kata ya Mgongo Wilayani humo.

Dkt Nchimbi ametoa agizo hilo mara baada ya kutembelea mnada huo ambapo wananchi wamelalamika kukosa huduma za vyoo na maji kwa kipindi kirefu huku halmashauri ikikusanya ushuru bila kuwaboreshea miundombinu ya mnada huo.

“Mkurugenzi nakupa mwezi mmoja hapa kuwe na vyoo bora vikiwa na matundu sita kwa ajili ya wananchi hawa pamoja na huduma za maji, kipindi cha mvua kinaanza, lazma muwajali wananchi hawa kwakuwa kipindupindu kinaweza kulipuka hapa”, ameeleza Dkt Nchimbi.

Ameongeza kuwa kwakuwa hakuna vyoo wananchi watajisaidia maeneo ya jirani na mnada na mvua zikianza zitatiririsha uchafu huo katika eneo la mnada na makazi ya wanakijiji cha Malendi na hivyo kusababisha mlipuko wamagonjwa hasa Kipindupindu,

Dkt Nchimbi amesema Mkurugenzi huyo ajenge vyoo vyenye matundu sita pamoja na kuvuta huduma za maji kwakuwa maji husaidia usafi wa eneo hilo na kupunguza uwezekano wa magonjwa hayo.

“Halmashauri mna jukumu la kuhakikisha mnada huu una miundombinu yote hasa ya maji na vyoo kwakuwa mnakusanya ushuru pia kumbukeni kuhakikisha huduma zinapatikana vizuri mnadani hapa”, ameelekeza Dkt Nchimbi.

Aidha amewataka Wakurugenzi wa halmashauri za Mkoa wa Singida kwa kushirikiana na idara za usafi wa mazingira na Wakala wa barabara vijijini (TARURA) wanahakiki njia na mitaro ya kupitisha maji ili mvua zisilete maafa pamoja na kuhakiki mabwawa ili baada ya mvua kuisha waweze kuvuna maji ya kutosha.

Dkt Nchimbi ameeleza kuwa mvua za msimu uliopita zilileta maafa ya kipindupindu hivyo hatarajii kwa mvua za msimu huu kuleta tena magonjwa kwakuwa wakurugenzi wametahadharishwa mapema uwepo wa mvua za wastani na juu ya wastani.

Ameongeza kwa kuwashauri wananchi kuimarisha makazi yao ili yaweze kuhimili mvua hizo pamoja na kujenga vyoo bora ili wasipate magonjwa hasa kipindupindu.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Iramba Marietha Kasongo amesema amelipokea agizo hilo na kuongeza kuwa mwezi mmoja unatosha kujenga vyoo hivyo na kufikisha huduma za maji mnadani hapo.

Amesema halmashauri ilikuwa na mpango wa kujenga vyoo na kuvuta maji mnadani hapo hivyo agizo la Mkuu wa Mkoa limewaamsha ili waweze kutekeleza mipango yao kwa haraka zaidi.

Awali Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini imetangaza kuwa Mkoa wa Singida unatarajiwa kupata mvua za wastani na juu ya wastani, aidha wastani wa mvua kwa Mkoa wa Singida ulikuwa ni Milimita 500 mpaka 850.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.