• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

DR.SAMIA AWASHIKA MKONO WATOTO MAHITAJI MAALUM SINGIDA.

Posted on: March 30th, 2025

Kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mkuu wa Mkoa wa Singida,Mheshimiwa Halima Dendego,amekabidhi  msaada wa vyakula na vinywaji kwa vituo viwili vya kulelea watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu mkoani Singida, ikiwa ni sehemu ya kusherehekea Sikukuu ya Eid El-Fitr.

Vituo vilivyonufaika na msaada huo ni Thanaratul-Qadiria, kinachoongozwa na Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issah Nassoro, kilichopo mtaa wa Majengo, pamoja na kituo cha Malaika wa Matumaini kinachoendeshwa na Kanisa Katoliki, Jimbo la Singida, huku msaada huo ukiwa na thamani ya jumla ya Shilingi milioni tano.

Akikabidhi msaada huo, Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego, alisema Dk. Samia ametoa mchango huo kama ishara ya mshikamano na upendo kwa watoto hao, ili nao wajione sehemu ya jamii kama watoto wengine wanaoishi na familia zao.

"Rais ameona umuhimu wa kushiriki na ninyi katika furaha ya Sikukuu ya Eid, ili msijisikie wapweke.. hili ni jukumu letu sote kama jamii kuhakikisha mnapata malezi bora na faraja tele ya maisha," alisema Dendego.

Aidha, aliwataka wadau wa maendeleo na watu wenye mapenzi mema, kujitokeza zaidi kusaidia vituo vya kulelea watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu, ili kuhakikisha wanawalea na kiwaweka kwenye mazingira bora, yanayowapa matumaini ya maisha thabiti, ya baadaye.

Msaada uliotolewa katika vituo hivyo ni mchele, mafuta ya kupikia, sukari, sabuni, vinywaji baridi, maji pamoja na mbuzi wanane, watakaotumika kwa ajili ya kitoweo cha Sikukuu ya Eid El-Fitr.

Viongozi wa vituo hivyo, akiweno sheikh wa Mkoa wa Singida Issah Nassoro, walishukuru kwa msaada huo, wakieleza kwamba utasaidia kuboresha lishe na furaha ya watoto waliopo katika vituo vyao.

Akizungumza baada ya tukio mtoto Nasibu Waziri, kwa niaba ya  watoto waliopokea msaada huo  ameonyesha furaha na kumshukuru Rais  Samia kwa upendo wake, huku akiahidi kuwa watakua  wakimwombea kwa Dua, na kuendelea kusoma kwa bidii ili kufanikisha ndoto zao za baadaye.

Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ni kipindi ambacho waumini wa dini ya Kiislamu hutumia kufanya ibada, kutafakari na kusaidiana, ili kuimarisha uhusiano wao na Mwenyezi Mungu pamoja na jamii inayowazunguka.


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.