• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

Posted on: May 12th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Daktari Fatuma Mganga ametoa maagizo ya kuhakikisha Halmashauri zote zinafunga mashine za kuongeza virutubishi vya lishe ili kuhakikisha wananchi pamoja na wanafunzi mashuleni wanapata chakula chenye virutubisho muhimu kwa ajili ya kuimarisha afya zao.

Ameyasema hayo leo Mei 12,2025 katika kikao cha Kamati ya lishe cha Mkoa kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida kikihusisha  wadau mbalimbali wakiwemo wajumbe wa Kamati hiyo,wakurugenzi wa Halmashauri na Manispaa,na wadau kutoka Taasisi mbali mbali.Sambamba na hilo amepongeza matumizi mazuri ya mfumo wa GoTHOMIS kwa ajili ya ukusanyaji mzuri wa taarifa mbalimbali za afya  na kutoa maagizo ya kuhakikisha wananchi wanahamasishwa kujiunga na matumizi ya Bima ya Afya.

Katibu wa kikao hicho Dkt.Victorina Ludovick(Mganga Mkuu wa Mkoa)amewasilisha utekelezaji wa maazimio mbali mbali katika kikao ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya mashine za kuongeza virutubishi kwenye unga wa mahindi,kuhakikisha wakinamama wajawazito wote wanapimwa wingi wa damu kwa asilimia zaidi ya 95,kufanya uchambuz iwa kina kwenye utoaji wa huduma ya Vitamini A kwa wakina mama waliojifungua na utoaji wa dawa za minyoo kwa watoto chini ya miaka mitano na kuandaa taarifa inayoonyesha vituo vyenye changamoto katika utoaji wa huduma hizo.

Kadhalika amesema kuwa kila shule inapaswa kuainisha kiasi cha chakula kilichovunwa ukilinganisha na kiasi cha mazao kilicholimwa kwenye shule husika.

Kwa upande wa matumizi ya teknolojia katika utaoaji wa huduma,Dkt.Victorina amesema kuwa hali ya matumizi ya mfumo wa Serikali wa Taarifa za uendeshaji wa huduma za Afya,(GoTHOMIS) katika vituo vya afya ambapo matumizi yake yamefikia asilimia 95.Pia utekelezaji wa agizo la ufungaji wa mfumo mpya wa  Centralized GoTHOMIS ambapo vituo 258 kati ya 272 vimetekeleza.

Akiwasilisha Viashiria vya upatikanaji wa lishe Mkoani Singida ,Afisa lishe mkoa Bi.Teda Sinde amesema lishe hupimwa kwa vigezo mbali mbali ikiwemo idadi ya wakina mama waliojifungua na kipata matone ya Vitamin A,idadi ya watoto walionyonya maziwa ya mama ndani ua lisaa limoja baada ya kuzaliwa,idadi ya wajawazito waliohudhuria kliniki ya wenye mimba  chini ya wiki 12,hali ya utoaji wa vyakula vilivyoongezea virutubishi katika shule za msingi,hali ya mavuno katika mashamba ya Shule za Msingi ikiwemo karanga,alizeti,maharage,kunde,mahindi,mtama na mpunga.

Akifunga kikao hicho kwa niaba ya Mwenyekiti wa kikao Bw.Romwald Mwendi amesema kuwa ni vema kufatilia suala la takwimu za afya ili kuhakikisha taarifa zinazowasilishwa zinakua na usahihi na kurahisisha utafutaji wa suluhu pale tatizo linapoonekana na kurudisha nyuma maendeleo ya upatikanaji wa lishe kwa wananchi.Pia amesema kuwa Serikali imetoa kiasi cha Shilingi Bilioni 2.7 kwa ajili ya kumalizia miradi ya ujenzi wa majengo ya afya na elimu ambayo yalikua hayajakamilika ikiwemo madarasa,zahanati,mabweni nakadhalika kwa lengo la kuhakikisha kuwa huduma zinawafikia wananchi katika mazingira mazuri.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.