• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

KAMATI YA USHAURI NA KLINIKI YA SHERIA YAZINDULIWA SINGIDA

Posted on: May 19th, 2025

 Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe.Halima Dendego amezindua rasmi Kamati ya Ushauri wa Kisheria ngazi ya Mkoa na Wilaya na Kliniki ya Sheria bila malipo kwa Wananchi wa Mkoa wa Singida leo tarehe 19 Mei, 2025 katika viwanja vya Stendi ya zamani Manispaa ya Singida.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mgeni Rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Halima Dendego ameipongeza Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kuuchagua Mkoa wa Singida na kuja kuzindua Kamati ya Ushauri wa Kisheria ngazi ya Mkoa na Wilaya kwa kuwa ni fursa kwa wananchi wa Mkoa huo kutatuliwa changamoto mbalimbali za kisheria zinazowakabili.

"Kipekee naishukuru Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Kamati ya Ushauri wa Kisheria ngazi ya Mkoa na Wilaya kwa kunifikiria na kunipa wajibu huu mkubwa wa kuwa Mgeni Rasmi katika Halfa hii ya Uzinduzi wa Kamati na Kliniki ya Sheria bila malipo katika mkoa wetu”.Amesema Mhe. Dendego.

Mhe. Dendego amesema kuwa kuzinduliwa kwa Kamati hiyo pamoja na masuala mengine, kutasaidia Kupunguza mashauri au migogoro dhidi ya Serikali, kuwawezesha Mawakili wa Serikali kusimamia Utawala wa Sheria katika maeneo yao, Kuwawezesha Mawakili wa Serikali kushirikiana na wadau wengine katika kutatua kero za wananchi na kupunguza malalamiko ya kisheria kutoka kwa wananchi.

“Naomba kukuahidi Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwa nitazisimamia Kamati hizi kikamilifu ili ziweze kuwa na tija katika mkoa wetu.” Amesema Mhe. Dendego

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Singida ametoa wito kwa Wananchi wa Mkoa huo kujitokeza kwa wingi katika Kliniki ya Sheria bila malipo ili waweze kupata huduma mbalimbali za kisheria hususani katika masuala ya mirathi, Ardhi, ndoa na Ajira.

"Nitoe wito kwa Wananchi wa Singida kujitokeza kwa wingi katika Kliniki hii kwani Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imekuja na Wataalamu waliobobea katika masuala ya Kisheria na wanatoa huduma hii bure kabisa.”Amesema Mhe. Dendego

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza S. Johari amesema kuwa kuzinduliwa kwa Kamati ya Ushauri wa Kisheria ngazi ya Mkoa na Wilaya pamoja na Kliniki ya Sheria kwa Wananchi wa Mkoa wa Singida ni mojawapo ya hatua za Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika kusogeza huduma za kisheria karibu zaidi na wananchi.

Aidha, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ameeleza kuwa moja ya njia inayotumiwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwajibika kwa wananchi ni kutoa ushauri na msaada wa kisheria kwa wananchi kwa kutumia Kamati za Ushauri wa Kisheria kwa ngazi ya Mkoa na ngazi za Wilaya.

"Lengo kuu la uanzishwaji wa Kamati za Ushauri wa Kisheria kwa ngazi ya Mkoa na Wilaya ni kurahisisha usimamizi wa utoaji wa ushauri wa kisheria kwa wananchi katika maeneo husika”. Amesema Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

 Uzinduzi wa Kamati ya Ushauri wa Kisheria kwa Mkoa wa Singida utafuatiwa na Kliniki ya sheria kuanzia tarehe 19 hadi 25 Mei, 2025 ambapo huduma za ushauri wa kisheria zitatolewa kwa wananchi bila malipo, ambapo amesisitiza Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali itatoa huduma hizo kwa ubora.

Kliniki hiyo ya Sheria inalenga kusogeza huduma za sheria karibu na wananchi, kuwaongoza wananchi katika taratibu za kupata haki zao pale zinapovunjwa au zinapoonekana kuelekea kuvunjwa, kutoa elimu ya sheria kwa wananchi na kuongeza ushirikiano miongoni mwa Mawakili wa Serikali na Mawakili wa Kujitegemea, na kuepusha au kupunguza mashauri yasiyo ya lazima.




Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MIRADI WILAYANI ITIGI KUNUFAISHA MAELFU YA WANANCHI.

    May 21, 2025
  • KAMATI YA USHAURI NA KLINIKI YA SHERIA YAZINDULIWA SINGIDA

    May 19, 2025
  • MAGARI MAPYA WILAYANI,UTENDAJI KUIMARIKA!

    May 19, 2025
  • SERIKALI KUU YAMWAGA FEDHA ZA MIRADI MANISPAA YA SINGIDA

    May 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.