• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Mfumo wa M-Mama wazindulia rasmi Mkoani Singida, Serukamba aagiza kutumika kupunguza vifo vya Mama wajawazito na mtoto.

Posted on: November 22nd, 2022

Halmashauri za Mkoa wa Singida zimetakiwa kutenga fedha katika mipango na bajeti zake kwa ajili ya gharama za usafiri wa dharura kwa Mama wajawazito na watoto wachanga.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba leo Novemba 22, 2022 wakati akifungua kikao cha Uzinduzi wa Mpango wa Usafirishaji wa dharura kwa akina Mama wajawazito, waliojifungua na watoto wachanga (M-Mama) kwa Mkoa wa Singida.

Rc Serukamba ameelekeza kwamba mfumo huo utakuwa ni msaada mkubwa kwa  wananchi wa Singida kwakuwa utasaidia kupunguza vifo vya  Mama wajawazito, wanaojifungua na watoto kwa kuweza kufikishwa Hospitali au vituo vya afya kwa wakati.

Amesema mpango wa huduma hiyo utaboresha zoezi la rufaa kati ya vituo vya kutolea huduma za Afya, hasa upatikanaji wa usafiri wa dharura kutoka kituo kimoja hadi kituo kinachoweza kutoa huduma ya viwango vya juu ambapo ameeleza kwamba utasaidia kupunguza changamoto ya upungufu kusubiria foleni ya magari ya wagonjwa.

“Kama tunavyofahamu huduma za Afya ya Mama na Mtoto hutolewa bila malipo, kwa hiyo hatua mbalimbali za kuhakikisha huduma bora zinapatikana katika Mkoa wetu wa Singida, ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya vituo vya kutolea huduma za Afya vinavyotoa huduma kamili za dharura na Upasuaji kutoka vituo vya huduma sita (6) mwaka 2020 hadi saba (7) mwaka 2022” amesema Serukamba

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba akisoma hotuba yake mbele ya washiriki wa zoezi la uzinduzi rasmi wa  Mfumo wa M-Mama uliyofanyika kimkoa katika ukumbi wa mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Kwa upande wake Mratibu wa afya ya uzazi na mtoto Mkoa wa Singida Christoweru Barnaba wakati akitoa wasilisho lake amesema mradi huo utasaidia kwa kiwango kikubwa kupunguza vifo vya mama na mtoto.

Aidha ameleeza kwamba  uwepo wa changamoto ya Upungufu mkubwa wa magari (Ambulance) za kubebea wazazi na wagonjwa wanaohitaji rufaa hasa Halmashauri ya Itigi, Mkalama, Singida, Ikungi kwa uwepo wa mradi huo utasaida kwa kuwa magari binafsi yatasajiliwa kwa ajili ya kupeleka wagonjwa.

Akimalizia wasilisho lake Christoweru ametoa wito kwa  mama wajawazito kuacha tabia ya kujifungulia nyumbani au njiani na badala yake wahakikishe wanafika hospitalini ili waweze kukutana na wataalamu.

Mratibu wa Afya ya uzazi na mtoto Mkoa wa Singida Christoweru Barnaba, akiwasilisha mada wakati wa uzinduzi huo.

Aidha Mkurungenzi  wa mfumo wa M-Mama Dolorosa Duncan kutoka Kampuni ya Vodafone  foundation amesema Serikali kwa kushirikiana na Vodacom inatekeleza mfumo wa rufaa na usafiri wa dharura – M-Mama ambao umefanyiwa majaribio katika Wilaya za mkoa wa Mwanza na Shinyanga na kuona unafanya kazi kwa ufasaha.

Hata hivyo Dolorosa ameendelea kueleza kwamba mfumo huo kwa sasa umeanza kutekelezwa katika mikoa ya Shinyanga Lindi Mororgoro Dodoma Tanga  na sasa Singida na Manyara ambapo utaendelea kutekelezwa katika mikoa yote ya Tanzania bara na Visiwani.

Mkurungenzi  wa mfumo wa M-Mama Dolorosa Duncan,akiwasilishamadawakati wa uzinduzi huo


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.