• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

MADIWANI WATAKIWA KUSIMAMIA MIRADI,MAPATO NA NIDHAMU KWA WATUMISHI

Posted on: January 15th, 2026


 Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego, amewataka madiwani wa Manispaa ya Singida na Halmashauri ya Wilaya ya Singida (DC) kuhakikisha wanasimamia ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa asilimia 100 pamoja na kubuni vyanzo vipya vya mapato, ili kuimarisha ujenzi na ukarabati wa barabara pamoja na miundombinu mingine muhimu ya kijamii.

Mhe. Dendego ametoa wito huo leo Januari 15, 2026, wakati akifunga mafunzo ya siku tatu kwa Waheshimiwa Madiwani yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa, yakilenga kuwajengea uwezo viongozi hao katika utekelezaji wa majukumu yao.

Akizungumza katika hafla ya ufungaji mafunzo hayo, Mhe. Dendego amesema madiwani wana wajibu mkubwa wa kusimamia ipasavyo ukusanyaji wa mapato ya halmashauri zao, akisisitiza kuwa mapato hayo ndiyo nguzo ya maendeleo katika sekta mbalimbali.

“Ukusanyaji wa mapato unatakiwa uwe wa asilimia 100. Ninyi madiwani ndiyo mnatakiwa kusimamia upatikanaji wa mapato haya, kwa kuwa ndiyo yanayosaidia ujenzi wa barabara, madarasa na miundombinu mingine muhimu. Haitakiwi kuwaambia wananchi wasilipe kodi; kodi hizi ni kwa maendeleo yao na ya nchi kwa ujumla,” amesema.

Kwa upande mwingine, Mhe. Dendego amewataka madiwani kuhakikisha usajili wa wanafunzi unafanyika kwa asilimia 100 katika kata zao, hususan kwa watoto wenye sifa za kuanza shule, na kusimamia kuhakikisha wanafunzi wote waliochaguliwa wanaripoti shuleni kwa wakati.

Aidha, amewakumbusha madiwani kuendelea kusikiliza na kushughulikia kero za wananchi, akisisitiza kuwa jukumu lao la msingi ni kuwahudumia wananchi na kusimamia maendeleo katika maeneo yao.

Mafunzo hayo ya siku tatu yaliyoanza Januari 13 hadi 15,2026 yalilenga kuwajengea uwezo madiwani katika masuala ya uongozi, usimamizi wa mapato, na uwajibikaji kwa jamii wanazoziongoza.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WATAKIWA KUSIMAMIA MIRADI,MAPATO NA NIDHAMU KWA WATUMISHI

    January 15, 2026
  • CHANGAMOTO ZA WAFUGAJI NA WAVUVI SINGIDA ZAANZA KUPATIWA UFUMBUZI

    January 10, 2026
  • WANANCHI WAGUSWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA KISHERIA MKOANI SINGIDA

    January 09, 2026
  • MIFUMO YA KIDIGITALI KUWAFUNGULIA MILANGO WAJASIRIAMALI

    December 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.