• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

MRADI WA MABWAWA YA KUTIBU MAJITAKA KUKAMILIKA OKTOBA,WANANCHI KUNUFAIKA

Posted on: September 23rd, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Fatuma Mganga, leo amefanya ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo ndani ya Manispaa ya Singida, ambapo alipata fursa ya kukagua Mradi wa Ujenzi wa Mabwawa ya Kutibu Majitaka unaotekelezwa katika eneo la Manga, Kata ya Mtipa.

Katika ziara hiyo, Dkt. Mganga sambamba na timu ya ufuatiliaji ya Mkoa walisomewa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo mkubwa na wa kimkakati, ambao unalenga kuboresha huduma za usafi wa mazingira na afya ya umma kwa wakazi zaidi ya laki moja wa Manispaa ya Singida.

Mradi huo unatekelezwa na Wizara ya Maji kupitia Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Singida (SUWASA), na unahusisha ujenzi wa mabwawa matano ya kutibu majitaka kwa teknolojia ya kisasa (anaerobic, facultative & wetlands), pamoja na maabara ya kupima ubora wa majitaka yaliyotibiwa, gari la kubeba majitaka, barabara na uzio wa kuzunguka eneo la mradi.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, hadi kufikia Septemba 2025, utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 71, huku mabwawa yote matano yakiwa tayari yamekamilika. Shughuli zinazoendelea ni pamoja na ulazaji wa mabomba ya kuunganisha mabwawa, ukamilishaji wa jengo la maabara, jengo la mlinzi na usimikaji wa nguzo za fensi.

Mradi ulianza kutekelezwa rasmi tarehe 16 Mei 2023, na unatarajiwa kukamilika tarehe 27 Oktoba 2025, kwa kipindi cha miezi 29 na siku 11.

Katika taarifa hiyo, ilielezwa kuwa zaidi ya wananchi 112,934 watanufaika moja kwa moja na mradi huo kwa kupata huduma bora za usafi wa mazingira. Aidha, mradi huo unatarajiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa uwezekano wa kuenea kwa magonjwa ya tumbo na kuhara yanayosababishwa na uchafuzi wa mazingira kutokana na utiririshaji wa majitaka usio rasmi.

Majitaka yaliyotibiwa yatatumika kwenye kilimo cha mboga mboga na matunda, hivyo kuongeza kipato kwa wananchi wa maeneo ya jirani. Vilevile, mradi unazalisha mbolea bora ya muda mrefu ambayo itapatikana kutoka kwenye mabwawa hayo, na inakadiriwa kudumu shambani kwa hadi miaka mitatu.

Zaidi ya hayo, eneo la mradi lina ukubwa wa meta za mraba 211,005, ambalo litahifadhiwa na kuendelezwa kwa upandaji miti na uboreshaji wa uoto wa asili, hatua itakayochangia kuimarisha hali ya hewa ya eneo hilo.

Dkt. Fatuma Mganga amepongeza hatua kubwa ya utekelezaji iliyofikiwa na kueleza kuwa Serikali ya Mkoa itaendelea kufuatilia kwa karibu miradi yote ya maendeleo ili kuhakikisha thamani ya fedha inaonekana na wananchi wanapata huduma bora kwa wakati.


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HALI YA HEWA YA MKOA WA SINGIDA YATAKIWA KUTUMIWA KAMA FURSA NA SIO KIKWAZO

    September 25, 2025
  • MRADI WA MABWAWA YA KUTIBU MAJITAKA KUKAMILIKA OKTOBA,WANANCHI KUNUFAIKA

    September 23, 2025
  • CHUO CHA UTUMISHI WA UMMA SINGIDA MBIONI KUHAMIA MAJENGO MAPYA.

    September 23, 2025
  • "MSITUMIE NYUMBA ZA IBADA KUHAMASISHA VURUGU":RC DENDEGO

    September 21, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.