• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

"MSITUMIE NYUMBA ZA IBADA KUHAMASISHA VURUGU":RC DENDEGO

Posted on: September 21st, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Halima Dendego amewaasa waumini kutumia vizuri majukwaa ya kanisani katika kuhakikisha amani inadumishwa na sio kuleta uchochezi na kuhamasisha vurugu ambayo matokeo yake husababisha ukosefu wa amani.

Ameyasema hayo leo Septemba 21,2025 katika kanisa la Uweza wa Bwana kata ya Minga akiwa kama Mgeni rasmi katika kongamano maalum la kuombea amani kuelekea Uchaguzi Mkuu.


Amesema kuwa waumini wanapaswa kujifunza na kujitahadhari  kwa kutumia mifano ya nchi za  jirani ambazo hazina amani kutokana na kukosa utulivu wa kisiasa ambao unapelekea wananchi kushindwa kujihusisha na shughuli za kiuchumi na uzalishaji mali ambazo hupelekea kukosa vyakula na kukumbwa na baa la njaa na vifo vingi.

"Amani katika Taifa ndiyo msingi wa kila kitu,hakuna maendeleo wala shughuli za kiuchumi bila amani,amani ikikosekana hakuna usalama,hatutoweza kuabudu wala kutafuta riziki.Hatuna Taifa lingine la kukimbilia bali sisi Tanzania ndio Taifa ndio kimbilio la wengine waliopoteza amani.

Hivyo ameiasa jamii kuikumbatia amani iliyopo bila kufuatisha maneno na msukumo wa watu mbalimbali wenye nia ovu ya kuharibu amani iliyopo kwa kutumia majukwaa ya kisiasa hususani katika kipindi hiki cha kampeni kuelekea uchaguzi mkuu.

"Ili kumaliza migogoro yote na kuitunza amani yetu iliyopo tusikubali kuwasililiza wale wote wanaoshawishi wananchi kutoshiriki katika uchaguzi mkuu mwaka huu.ili kuweza kuchagua viongozi bora wanaoona wanafaa kwenda kuwasilisha mapendekezo  na mahitaji yao Bungeni ni muhimu na haki yako kikatiba kushiriki zoezi la kupiga kura ifikapo siku ya Uchaguzi."amesema Mhe.Dendego.

Mhe.Dendego amehitimisha kwa kusema kuwa Serikali yetu haina dini bali inawaongoza wananchi ambao wana dini zao hivyo amewaomba waumini hao kuungana kufanya maombi kama hayo kwani suala la amani ya nchi ni jukumu la kila mmoja wetu.

Naye Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Uweza wa Bwana Mch.Barick Mapigano, amewaasa waumini kwenda kuwachagua Viongozi bora ambao ni Watumishi kutoka kwa Mungu ili kwenda kuwa Watumishi kwa wananchi kila mmoja kwa nafasi yake wakiwemo Madiwani,Wabunge na Rais  kwani uchaguzi ni jambo jema ambalo huondoa malalamiko baina ya watu,fadhaa na kukata tamaa kwani kupiga kura ni agizo kutoka kwa Mungu.

Kadhalika amewataka Wachungaji na waumini wengine  kuhakikisha hawakati tamaa ya kuhubiri amani kuelekea uchaguzi kwa kuhofia kupewa majina mabaya akisisitiza kuwa jambo jema zaidi ni amani na sio kuogopa kuihubiri amani na utulivu kwani endapo amani ikitoweka nafasi ya kuhubiri wala kusikiliza  mahibiri haitapatikana hivyo tuidumishe amani tuliyonayo na tusichoke kuwasisitiza wenzetu kuidumisha 

Akizungumza baada ya ibada,Bi.Miriam Israel amesema leo ni siku muhimu sana kwani ni ibada njema inayohubiri amani kwa nchi ya Tanzania na anaitumia siku hii na zile zijazo kuwahimiza waumini na wanajamii wenzake kuhakikisha wanashiriki uchaguzi mkuu mwezi Oktoba 2025 sambamba na kuhudhuria kampeni zinazoendelea ili kuweza kusikiliza sera mbalimbali za wagombea hao ili kuchagua zinazowagusa wananchi na kuwaletea maendeleo.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HALI YA HEWA YA MKOA WA SINGIDA YATAKIWA KUTUMIWA KAMA FURSA NA SIO KIKWAZO

    September 25, 2025
  • MRADI WA MABWAWA YA KUTIBU MAJITAKA KUKAMILIKA OKTOBA,WANANCHI KUNUFAIKA

    September 23, 2025
  • CHUO CHA UTUMISHI WA UMMA SINGIDA MBIONI KUHAMIA MAJENGO MAPYA.

    September 23, 2025
  • "MSITUMIE NYUMBA ZA IBADA KUHAMASISHA VURUGU":RC DENDEGO

    September 21, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.