• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

MWENGE WA UHURU 2021 WAPOKELEWA MKOANI SINGIDA, MIRADI 55 KUZINDULIWA

Posted on: July 20th, 2021

Miradi mbalimbali ya maendeleo yenye thamani ya shilingi bilioni 8.1 itakaguliwa na kuzinduliwa wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru zilizoanza leo  Julai 20, 2021 Mkoani Singida.

Akiongea leo wakati wa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge amesema kiasi hicho cha fedha kimetumika katika miradi 55 ya maendeleo katika Mkoa mzima.

“jumla ya miradi 55 inayohusu TEHAMA, Elimu Afya, mazingira maji biashara, barabara programu za rushwa, VVVU/UKIMWI, malaria na mapambano dhidi ya dawa za kulevya itatembelewa” amesema Mhe. Mahenge.

Amesema katika mbio hizo za Mwenge wa Uhuru miradi mipya 9 itazinduliwa, miradi  miwili itafanyiwa ufunguzi, sita itawekwa jiwe la msingi na 36 itakaguliwa na miradi miwili itatembelewa.

Aidha Mhe. Mkuu wa mkoa amebainisha kwamba kiasi hicho cha fedha kwenye miradi hiyo inatokana na michango ya wananchi kiasi cha sh.Bilioni 1.9, mchango wa Halmashauri kiasi cha sh.milioni 69.6 na kiasi cha sh. milioni 4.6 kutoka Serikali kuu.

Hata hivyo Mhe. Dkt. Mahenge ametoa wito kwa wanasingida wote kutumia kaulimbiu ya Mwenge wa Uhuru 2021 “TEHAMA ni msingi wa Taifa endelevu” kwa kuwajibika ili kuleta maendeleo ya mtu na Taifa kwa ujumla.

Amesema kutokana na umuhimu wa TEHAMA katika maendeleo ya Taifa mkoa umeendelea kusimamia zaidi ya mifumo 30 inayotumika katika mamlaka za Serikali za mitaa, Sekretarieti ya mkoa pamoja na  taasisi mbalimbali zilizopo ndani ya mkoa.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa amewataka wananchi wa Singida kujiunga na bima ya afya ili kukabiliana na gharama za matibabu.

Amewasihi wananchi kutumia lishe bora kwa afya imara ambapo kiwango cha udumavu kimeendelea kupungua hadi kufikia asilimia 29 mwaka 2018.

Mkoa umeendelea kutafuta suluhisho la tatizo la    ukondefu na upungufu wa uzito kwa watoto kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa lishe ambapo jumla ya vituo 99 vya huduma ya afya  vinavyotoa matibabu kwa watoto vimeanzishwa. Alibainisha  mkuu wa mkoa 

Mwenge wa Uhuru 2021, katika Mkoa wa Singida utakimbizwa kwa muda wa siku Tano (5), katika Wilaya Tano kwa kuanzia na Wilaya ya Iramba leo tarehe 20/07/2021 na utahitimisha mbio zake mnamo tarehe 24/07/2021 na tarehe 25/07/2021 utakabidhiwa Mkoa wa Dodoma. 

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.